HabariTech Profile picture
Jan 19 16 tweets 4 min read
📡Camera Iliyofichwa

Kila siku inayoanza na kuisha kuna watu wanalala Hotelini, lodge, nyumba za wageni na wengine wanakuwa wageni majumbani mwa watu.

Watu wanaofatilia sana movies na conspiracies huwa na wasiwasi wa kuwa recorded na camera zilizofichwa.

#HabariTech
📡Mara nyingi camera zilizofichwa huwa na lengo zuri la kudaka wezi au matukio ambayo yanaweza hatarisha usalama.

Na wakati mwingine camera hizi hufungwa kwa lengo la kutumika kudaka matukio ya faragha ili kusambaza kwa lengo la kumtia mtu aibu au kufanya blackmail.
📡Itakuwa vyema leo nikikujuza kuwa unaweza tumia smartphone yako kujua kama kuna camera zimefichwa katika chumba ulichopo.

MUHIMU: Njia hizi hazihusiana na kutambua camera ya Smartphone iliyofichwa.
1. Chunguza vizuri mazingira ya chumba ulichopo.

Ukiingia ofisini/bank na sehemu nyingine za muhimu kama utatizama vizuri juu utaona camera zimefungwa.

Hata ATM kuna camera imefungwa inayorekodi matukio yote.
Kuna wakati camera za hivi ndizo hufungwa kwenye baadhi ya vyumba hotelini ili kunasa matukio yanayoendelea ndani ya vyumba.

Mara nyingi huwa ni kwa nia nzuri, ila si jambo sahihi kufunga camera ndani ya vyumba.
Kwahiyo unapoingia chumba cha wageni jitahidi kuchunguza vizuri, iwapo utaona camera yoyote.

Una mawili aidha uondoke usitumie hicho chumba au waambie wazime camera zao unataka privacy yako.
2. Tumia simu yako

Hapa kuna njia mbili.

Moja, Washa wifi ya simu yako acha ifanye network scanning kama dakika moja hivi. Kuna aina ya CCTV camera zinakuwa connected na internet.

Hizi ni zile unaweza ona zinarekodi nini kutoka mahali popote duniani.
Camera hizi huonekana hata kwenye Wi-Fi ya simu. Hivyo kwa kutumia wifi ya simu yako utaweza kujua kama kuna camera ndani ya chumba hicho.

Kama inavyoonekana kwenye picha hapa chini
Mbili, Zima taa zote ndani ya hicho chumba kisha tumia camera ya simu yako (Ku)Scan chumba chote.

Iko hivi, Kuna camera ambazo hutoa infrared radiations kama ya remote za TV au decoder.

Ukilenga camera ya simu yako kwenye camera hizi kuna mwanga utatokea.
Ukiona mwanga wa hivyo sogea karibu uchunguze vizuri ni nini kinatoa mwanga huo. Mara nyingi huwa ni camera iliyofichwa.

Camera hizi hufichwa maeneo haya
.Fire detectors
.Vioo
.Makabati
.Mapambo
.Kona za chumba
.Feni
.Saa za ukutani
3. Chunguza vizuri vioo ndani ya chumba ulichopo

Kuna vioo aina mbili. Vya njia moja na njia mbili.

Kioo cha njia moja ni sawa na kila unatumia nyumbani kujiangalia asubuhi unapojiandaa kutoka.
Vioo vya hivi (kutegemeana na upana wa kioo) ukiweka kidole utaona kuna nafasi kati ya kidole chako na picha ya kidole kwenye kioo.

Kioo cha njia mbili, ni kile ambacho upande mmoja utaona reflection yako, lakini aliye upande wa pili anaona unafanya nini.
Kioo cha njia mbili ukiweka kidole utaona kinagusana moja kwa moja na kile kwenye kioo.

MUHIMU: Inategemeana sana na upana wa kioo.

Mtu aliyeko upande wa pili wa kioo cha njia mbili anaweza rekodi kila unachofanya bila wewe kumuona.
4. Mhoji vizuri mwenyeji wako

Hii ni haswa kwa wale wanaenda faragha kwa ajili ya mambo yao.

Iwapo huna imani na mwenzako, kabla hamjaanza mambo yenu basi tumia namna yote mshawishi simu zenu mziweka mahali pa wazi zionekane.
Pia usikubali ashike simu bila kujua nini anafanya. Itakusaidia kuepukana na aibu zisizo za lazima.

Hii yote ni kwa sababu faragha ni ya muhimu kwa kila mtu. Jali sana privacy yako itakulinda sana.
Usisahau kupakua magazine ya @HabariTech toleo 3 kujifunza mengi zaidi

Link 👇

habaritech.gumroad.com/l/habaritech3

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with HabariTech

HabariTech Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @HabariTech

Jan 11
🚀Thetan Arena MOBA

Leo tuzungumze kuhusiana na Game moja wapo unayoweza kulipwa kwa kuicheza. Game hii inaitwa Thetan Arena MOBA.

MOBA (Multiplayer Online Battle Arena). Hii ni gam ambayo unacheza kwa kupigana battles na watu wengine Online.

#HabariTech Image
🚀Kumekuwa na P2E games nyingi zilizoundwa hivi karibuni. Nyingi zikiwa na mfumo wa card based na nyingine trading based.

Thetan Arena inatumia mfumo wa battles (yaani kupiganisha characters ndani ya game).

Battles hizi zinapigwa mtandaoni kati ya character wako na wa adui yako Image
🚀Characters wa Thetan Arena tunawaita Heroes. Heroes hawa utawapiganisha katika teams.

Na kwa ushindi unaopata utazawadiwa tokens za game hii ambazo kwa sasa token moja ina thamani ya $4.
Read 26 tweets
Dec 28, 2021
✨Kwa sasa simu nyingine zinatumia sim card ile ya card ya kutoa na kuweka.

Ili mtu uwe na namba zaidi ya moja unalazimika kuwa na sim card zaidi ya moja.

eSim itakuja kuondoa hii tabu.

#HabariTech 🧵
✨eSim (Electronic Sim Card au Embedded Sim Card)

Hii ni sim card ambayo unaweza download ya mtandao wowote na kuitumia ndani ya simu yako. Nasema unaweza download kwa maana ya kwamba.

Ndani ya simu yako unakuwa na chip ambayo inafanya kazi kama hizi sim card za kawaida.
✨ili uweze kupata mtandao itakubidi uijaze na taarifa za mtandao husika unaotaka kutumia.

Kwa sasa ukiwa na namba moja ya Voda au Tigo kwenye sim card yako, huwezi ibadili hiyo namba bila kubadili sim card.
Read 7 tweets
Dec 27, 2021
Wengi sasa hivi mnatamani kuingia kwenye UX Designing. Inapendeza kuona watu kama @AbilMdone @mzabayuni na @iamKaga wanawapa motisha.

Ni rahisi kudrag & drop elements kufanya graphics designing ukidhani ni UX designing.
UX designing inahusiana na lengo la mtumiaji wa app au website yako. Haingii kwenye app au website kushangaza majo avutiwe na muonekano.

Anatumia website/app yako ili kufanyikisha jambo fulani.
Wengi tunakosea kudhani kwamba UI nzuri ni ile inayovutia tu machoni.

Ukweli ni kwamba UI nzuri ni ile mtuamiaji anaweza elewa na kutumia bila shida, ajiskie fahari kuitumia na imtongoze kuitumia.
Read 4 tweets
Nov 19, 2021
📡iOS ni Bora kuzidi Android mbali sana 👀

Hii vita tungewapa silaha nani atashinda? Tuachana na hayo tusifike huko.

Hii mada kila ikiwekwa mezani mashabaki wa hizo OS huongelea sana kwamba wanayotumia wao ni bora.

Je, Ni kweli?

#HabariTech
📡Najua kwamba kuna mtu tayari anajizuia sana mpaka amalize kusoma ndipo ajibu.

Kuwa mpole bro/sis maisha sio vita 😁.

Binafsi mimi ni shabiki mkubwa wa Android na huwezi nibadilisha kwa lolote, ila pale ambapo utaalamu utatumika ukweli lazima usemwe.
📡Kwa sababu hiyo kwa kujiamini kabisa naweza kusema kwamba iOS ni bora kuzidi Android kwa mtumiaji wa kawaida wa simu.

Swali tukiacha liwe na mjadala kwamba ipi bora kuna vitu lazima utasikia kutoka pande zote mbili.
Read 22 tweets
Nov 18, 2021
Sio expert sana upande wa engineering ila naweza jibu hivi.

Sidhani kama quantum computing itakuja kuuzwa kwa watumiaji wa kawaida kama mimi na wewe.

Labda sio kwa miaka 100 ijayo 😁 watumiaji wa kawaida kama mimi na wewe tunahitaji quantum computing ability kwa ajili ya nini?
Anyway tuseme itakuwa available kwa consumers nani yuko tayari kulipia gharama za kumiliki na kumaintain running costs za quantum computer?

Kila mtu anatamani kuwa na kifaa chenye super conducting ability, ila nikiwaza huo umeme wake 😂.
Alafu kuna ishu ya cooling. Kifaa cha quantum kinahitaji kuwa na cooling system iliyopo efficient sana na inaweza kuwa kubwa sio kawaida.

Kitu ambacho kufit kwenye PC ni meh! 🤔

Quantum computers zina advantage kunwa zikitumika kwenye sehemu kama data centers.
Read 5 tweets
Nov 8, 2021
📡Tabia zinazo haribu PC yako kwa haraka.

Sisi sote tunapenda kuona vifaa vyetu kama PC zikidumu kwa muda mrefu, lakini mara nyingi huwa zinaharibika mapema tofauti na mategemeo yetu.

#HabariTech Image
📡Huenda tabia zetu na namna tunatumia hivi vifaa ikawa ni sababu ya hizi mashine kuharibika haraka Image
📡Hakuna kitu kinachodumu milele na hasa vifaa vya elektroniki. Watengenezaji wa vifaa hutengeneza vifaa wakiwa na malengo kwamba kwa matumizi sahihi hicho kifaa kitadumu kwa miaka kadhaa.

Muda huo huwa sahihi ukitumia ipasavyo kwa usahihi.

Nini kinaua PC yako mapema?
Read 23 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!

:(