HabariTech Profile picture
Mar 15 33 tweets 7 min read
👽Russia hawataweza kuvuka vikwazo vya Teknolojia

24 February 2022, baada ya Russia kuvamia Ukraine, serikali ya Marekani ilitangaza vikwazo vya kwanza Russia.

Katika vikwazo hivyo vilikuwemo vinavyogusia teknolojia.

#HabariTech
👽Moja ya kikwazo kilisema, "Kuzuia zaidi ya nusu ya uagizaji wa Russia kuingiza teknolojia ya juu nchini mwao, Kuzuia Russia kupata pembejeo muhimu za kiteknolojia, Kudhoofisha msingi wao wa viwanda...
👽...na kudhoofisha matarajio ya kimkakati ya Russia ya kuwa na Ushawishi katika jukwaa la ulimwengu." -mwisho wa nukuu.

Inawezekana ilionekana ni kikwazo kikubwa kwa muda huo. Ila ni kidogo sana ukilinganisha na yaliyofata baada ya hapo.
👽Mambo yalizidi kuwa mabaya kwa Russia, baada ya mamilioni ya watu kuonyesha kutofurahishwa na anachokifanya Russia.

Serikali za dunia na kampuni binafsi zilichukizwa na kitendo hiki na walianza ichukulia Russia hatua.
👽Vikwazo vilivyotangazwa na serikali za dunia na hatua zilizochukuliwa na kampuni binafsi iwapo vitasimama, kuna uwezekano mkubwa uchumi wa Russia utayumba vibaya mno.

Upande wa Teknolojia hii hali itafanya Russia irudi nyuma zaidi ya miaka 10.
👽Russia anatumia teknolojia kupigana vita zake. Kuanzia Cyberattacks mpaka vifaa vya kivita anavyotumia kuharibu miundo mbinu ya mawasiliano huko Ukraine.

Vikwazo vya mwanzo vya US viligawanyika katika makundi mawili.
👽Moja, ilikuwa katika mali zilizo milikiwa na serikali. Kikwazo hiki kilizuia kuagiza vipuli vya vifaa vya kivita, hakuna user manual za vifaa kwenda Russia wala misaada ya kifedha inayohusu teknolojia ya vifaa vya vita.
👽Hii ina maana ya kwamba Russia hatakiwi kupokea tech yoyote iliyoundwa US bila kibali maalumu cha serikali.

Mbili, Watu wasio husika na jeshi kikwazo hiki kina maana hawataweza kupata vitu kama semi conductors, vifaa vya mawasiliano, huduma za usalama, avionics, sensors n.k.
👽EU, Korea Kusini na Japan pia waliweka vikwazo vinavyo endana na hivyo kwa namna yao.

Japo kwa nchi kama Korea Kusini hawakuweka vikwazo vigumu kwa kampuni zoa.

Samsung bado aliendelea kupeleka simu zake nchini Russia.
👽Waziri mkuu wa Italy pia alipendekeza bidhaa za starehe kama bidhaa za Gucci zisiwepo katika orodha ya vikwazo.

Mambo yalienda vizuri, lakini Russia alipozidisha uvamizi, mambo yalianza kubadilika.
👽Kampuni Binafsi kama Samsung na Prada wakaona ni bora wakafuata serikali za zilichofanya na kuacha kupeleka bidhaa zao nchini Russia.

Hata walionunua nishati kutoka Russia wakaona ni bora kuachana na zoezi hilo na kutafuta njia mbadala.
👽Kilichofuata ni kampuni za usafirishaji kuacha kutoa huduma yao Russia.

Hizi ni Maersk, FedEx na DHL.

Hii imepelekea kampuni za magari kama Ranault kushindwa endeleza huduma nchini Russia, hivyo kusimamisha utoaji huduma.
👽Orodha ya kampuni zinazoacha kutoa huduma kwa Russia inazidi kuongezeka.

Hata kampuni za ndege kama Airbus na Boeing wameacha kutoa huduma zao kwa Russia.

Kampuni hizi mbili wameacha kuuza ndege zao Russia, pia hawasafirishi tena vipuli kwenda Russia.
👽Kushindwa kupokea vipuli vya ndege pamoja na wataalamu na maelekezo ya matengenezo ya ndege kutafanya baadhi ya ndege kushindwa kuendelea na kazi ndani ya wiki chache.

Haya ni maoni yaliyotolewa na wataalamu kutoka Amadeus na Sabre.
👽Amadeus na Sabre ni kampuni zinazoongoza kwa kuuza tiketi za ndege dunia nzima.

Software za kampuni hizi zinatumika na kampuni za Russia kama Aeroflot zinatumia kuendesha biashara zao pamoja na kampuni za nje ambazo zinamiliki na...
👽...kukodisha takribani ndege 515 kati ya 980 zinazotumika na kampuni za ndege za Russia.

Kwa maana hiyo zaidi ya nusu ya ndege za abiria zilizopo Russia itatakiwa zirudi kwa wamiliki wake nje ya nchini kabla ya mwisho wa mwezi huu.
👽Upande wa magari na malori, karibu brand kubwa zote zinaacha kutoa huduma nchini Russia.

Kampuni kama Volvo, Mercedes, Volkswagen, Toyota, Renault na Ford zimeacha kuuza na kutoa huduma nchini Russia.

Pia wamefunga viwanda vyao nchini humo.
👽Ili ujue hii kitu inawaumiza kiasi gani Russia nikwambie hivi, "95%" ya vipuli vya magari nchini Russia vinaagizwa kutoka nje.

Bila kampuni ya usafirishaji kama Maersk, watengenezaji vipuli hawana budi ila kuacha kupela vipuli nchini Russia.
👽Upande wa consumer electronics, orodha hii ina kampuni kama Apple, Samsung, Dell na HP.

Katika biashara kubwa zinazotoa huduma kuna Microsoft, SAP na Oracle wameacha kutoa huduma mpaka za huduma kwa wateja.
👽Kampuni za malipo kama PayPal wameacha kabisa kutoa huduma yao nchini Russia, wakati huo huo Mastercard, Apple pay, Google pay na Visa wamepunguza huduma zao kwa kiasi kikubwa.
👽Mpaka sasa viwanda vingi nchini Russia vimeacha kufanya kazi. Waliobaki wanalazimika kubadili miundombinu ili kuendelea na kazi.

Kulingana na bloomberg, watu 3 milion wa Russia wanafanya kazi katika kampuni za nje au zinazoshirikiana na kampuni za nje kutoa huduma zao.
👽Kwa maana hiyo hawa watu 3 milion wapo katika hatari ya kupoteza kazi zao.

Hili jambo pia litaua biashara ndogo ndogo nchini humo.

Hii ni kwasababu hizi biashara aidha zinasambaza bidhaa zao kwa biashara kubwa au zinategemea bidhaa kutoka biashara kubwa za nje.
👽Hata kampuni zenye high-tech huko Russia zinategemea teknolojia ya nje.

Vitu kama roboti za viwandani kutoka Germany, Factory Automations kutoka US na Japan, hata kampuni za kuzalisha nishati za Russia zinategemea vifaa na software kutoka nje.
👽Swali ni je, hizi kampuni zitaweza kuendelea kufanya kazi?

Wakati haya yote yakiendelea, bado Russia wakapigwa tena na kitu kizito. Russia hatoweza kupokea kabisa Processor chip zenye ubora wa hali ya juu.

Walichobaki nacho ni consumer grade chip.
👽Intel & AMD walitangaza kuacha kupeleka Russia na Belarus processor za viwandani.

Zile zinazotumika kuendesha mitambo ya viwandani. Hizi ni pamoja na processor za servers na PC.

Hapa wanaguswa watu wa gaming PC, servers na supercomputers za Jeshi.
👽Nokia na Ericsson wameacha kuuza vifaa vya mtandao nchini Russia.

Huawei na ZTE bado hawajatoa tamko, lakini hawataweza kuuza vifaa vinavyotumia teknolojia zilizozuiliwa.

Vifaa hivi ni kama ASML machines havitatakiwa kuuzwa kwenda Russia.
👽Hii ina maana kwamba watoa huduma za mitandao ya simu watalazimika kubadili teknolojia waliyonayo na kuanza nunua teknolojia mpya kutoka China.

Russia sio kati ya nchi zenye uhitaji mkubwa wa processor chip kwa kuwa wao hununua vifaa vilivyopo tayari kwa matumizi.
👽Hivyo watu wanaweza pata intel processor katika laptop za Huawei au Qualcomm chip katika simu za Xiaomi.

lakini kitu chochote complex zaidi ya hapo kama processor kwa ajili ya vifaa vya jeshi hawataweza kupata.
👽Maabara zenye ubora zaidi Russia wana uwezo wa kutengeze processor chip kufikia 65nm tu. Hizi ni processor ambazo hazina uwezo mkubwa.

Zinatumika kwa kazi ndogo ndogo kama card za bank na milango zinazotumia electronic chip.
👽Kampuni mbili kubwa zinazofanya Chip Design nchini Russia Baikal Electronics na MLICT wanawatumia TSMC kama kiwanda cha kufanya manufacturing.

TSMC pia wametangaza kuwa wanaacha kufanya kazi na Russia.
👽Baadhi ya drones za jeshi za Russia zilizokamatwa Ukraine zimegundulika kutumia teknolojia ya nje kwa kiasi kikubwa.

Vitu kama Camera, Sensors mpaka Motors.

Labda Russia wanaweza kwenda China kuanza tumia Teknolojia za huko.
👽Lakini hata hiyo pia itakuwa ngumu kwa kuwa kampuni kama SMIC ya china pia wanatumia teknolojia ya nje ya China kuunda baadhi ya vifaa vyao.

Hivyo nao wanaweza kusiti kwa kuogopa kufungiwa teknolojia hizo na kampuni za nje.
Ninachoona ni kwamba Putin hakujiandaa na vikwazo vya namna hii. Jambo hili litapelekea kuyumba sana kwa uchumi wa Russia.

Lakini ngoja tusubiri kuona nini kitafata baada ya vita kuisha.

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with HabariTech

HabariTech Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @HabariTech

Mar 15
🎁T O R R E N T S, Zinafanya vipi kazi?

Naweka dau langu kwamba ukisikia torrents, kitu kinakuja kichwani mwako ni software, video au audio za wizi (Pirated Files).

Uko sahihi lakini, torrent protocol haihusiana na hivyo tu.

#HabariTech Image
🎁Torrents ni nini?

Kwanini pirates wanatumia torrents kusambaza na kupakua files zao?

Huduma nyingine za internet zinazoendana na torrents kwanini hazitumiki katika sharing ya pirated files?

Haya maswali yote yanapatiwa majibu kupitia Bittorrent protocol. Image
🎁Unapofungua browser ili kuperuzi mtandao, browser inatuma request kwenda kwenye server yenye IP address ya website unayotaka kuifikia.

Request hii inaenda kuiomba server ikupe HTML za hiyo website ili uweze kuiona na kufanya kitu unataka. Image
Read 28 tweets
Mar 14
🍿Nini Kiliwakuta Founders wa Pirates Bay

Pirates bay ni kati ya website bora za kufanya piracy ya Games, Softwares, Movies, Music na aina nyingi ya files zinazokuwepo online.

Ni website ambayo iko kinyume na sheria za hakimiliki na haikutakiwa kuwepo.

#HabariTech
🍿Kampuni nyingi na wanasheria duniani wamejaribu sana kuhakikisha website hii haipatikani mtandaoni bila mafanikio.

Kwa kuwa content zinazokuwepo huko hazikutakiwa kuwepo na mara nyingi zinawakosesha mauzo kwa kuwa ni usambazaji wa content usio sahihi.
🍿Kuna miaka ya nyuma waliwahi fanikiwa kuiondoa online. Bahati mbaya mafanikio yao hayakudumu kwa muda mrefu.

Saa chache baada ya kuondolewa online website ya Pirates bay ilirudi online. Hivyo wakaona wabadili namna ya mashambulizi yao.
Read 41 tweets
Jan 24
🚀Sifa Kuu ya MATAPELI

Kwa sasa teknolojia imefanya kupata pesa iwe rahisi sana, lakini kupoteza ni rahisi zaidi 😁.

Kutapeliwa ni dakika 0.

Kila unapogusa mtandaoni sasa hivi kuna haya maneno NFT, Cryptocurrency, Bitcoin.

Lengo ni PESA.
🚀Bahati mbaya wengi mnaishia kuumia kwa sababu mnakosa maarifa.

Mnaingia kichwa kichwa katika biashara msizoelewa haswa ziko vipi.

Kwa sababu hiyo unajikuta unajitapeli wewe mwenyewe. Ulikosea mwanzo kutotaka kusoma inakuaje wengine wanapata faida.
🚀Siri kubwa ya matapeli hata sio kubwa kivile. Ila tu kwa kuwa wengi hatuumizi akili huwa tunaipita tu.

Tapeli guru kabisa ana siri moja.

Kipindi ambacho dhahabu inapatikana kwa wingi yeye huwa hajishughulishi na uchimbaji.

Image Credit: @MaujanjaCrypto
Read 9 tweets
Jan 24
⚡Namna ya (ku)bypass restrictions za Channels na bots telegram

Kila mara whatsapp isipopatikana watu wengi hutumia telegram kwa muda.

Ukiacha hivyo telegram imekuwa sehemu nzuri ya kuendesha biashara kama anavyofanya @itzjacton na group la Soko Letu

#HabariTech
Au wanavyofanya @CipherdotM na channel yao ya movies. Kwa wengine telegram ni sehemu ya kupakua miziki ya Spotify, YouTube au Apple Music bila kuwa na account katika platform hizo.

Na wengine wanatumia kupakua movies za Netflix ama Amazon Prime
Bahati mbaya channel & bots nyingi zinazotumia majina na content za kampuni kubwa huwa zinafungiwa na telegram kwa sababu ya ukiukaji wa hakimiliki (copyright infringement).

Telegram wapo kulinda maslahi yao na ya kampuni nyingine, hivyo ni lazima wafanye hivi.
Read 7 tweets
Jan 23
C I A

Confidentiality, Integrity & Availability hizi ni kama muongozo wa usalama wa aina yoyote, ili kulinda taarifa zinazotunzwa au kutumwa dhidi ya mtu asiye husika.
Confidentiality, inahakikisha kwamba mtu asiyetakiwa kuwa na access hapati hiyo access. mfano account yako ya twitter inalindwa na password yako.

Password unayoijua wewe na kuiweka siri ndiyo confidentiality yenyewe. Maana yake ili mt apate access lazima umpe hiyo password.
Integrity, account yako ya twitter ikatokea imedukuliwa alafu tweets zikawa tofauti na tulivyokuzoea tutajua sio wewe.

Hapo integrity imepotea. Kwahiyo integrity ni ukweli na kuaminika kwa data. Mtu asiye ruhusiwa ku access system hatakiwi kuweza badili data ili integrity iwepo
Read 5 tweets
Jan 19
📡Camera Iliyofichwa

Kila siku inayoanza na kuisha kuna watu wanalala Hotelini, lodge, nyumba za wageni na wengine wanakuwa wageni majumbani mwa watu.

Watu wanaofatilia sana movies na conspiracies huwa na wasiwasi wa kuwa recorded na camera zilizofichwa.

#HabariTech
📡Mara nyingi camera zilizofichwa huwa na lengo zuri la kudaka wezi au matukio ambayo yanaweza hatarisha usalama.

Na wakati mwingine camera hizi hufungwa kwa lengo la kutumika kudaka matukio ya faragha ili kusambaza kwa lengo la kumtia mtu aibu au kufanya blackmail.
📡Itakuwa vyema leo nikikujuza kuwa unaweza tumia smartphone yako kujua kama kuna camera zimefichwa katika chumba ulichopo.

MUHIMU: Njia hizi hazihusiana na kutambua camera ya Smartphone iliyofichwa.
Read 16 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!

:(