#AfyaSwahili | OCTOBA - MWEZI WA UELEWA JUU YA SARATANI YA MATITI

➡️Uzi maalumu wenye jumbepicha ili kusaidia wanawake wapate kufahamu dalili za kansa

➡️Tafadhali sambaza isaidie wengi

Credit: Know Your Lemons

#BreastCancerAwarenessMonth
➡️Saratani ya titi ni kati ya saratani zinazowaathiri zaidi wanawake. (Namba 2 chini ya saratani ya shingo ya kizazi)

➡️Mwaka 2020 Tanzania kulikuwa na wagonjwa wapya 3992 wa saratani ya matiti (hawa ni wale waliofika kwenye vituo vya Afya) wengi huchelewa tiba

Uelewa ni muhimu
➡️Kuwa na uelewa kuhusu mwili wako na kuweza kugundua mabadiriko ni moja ya njia bora ya kulinda afya yako.

➡️Hii ina umuhimu mkubwa hasa linapokuja suala la matiti kwa wanawake.

Kwa wastani mwanamke 1 kati ya 8 huwa na uwezekano wa kupata saratani ya matiti kwa maisha.
KUCHUNGUZA SARATANI YA MATITI
1⃣Kujichunguza mwenyewe mara kwa mara kwa mara.
2⃣Uchunguzi wa kitabibu wa matiti kila mwaka.
3⃣Wanawake wote wenye umri kuanzia miaka 21 wajichunguze matiti yao siku ya 5-7 baada ya kumaliza hedhi mbele ya kioo.
DALILI 1 - UGUMU KWENYE TITI
➡️Saratani huweza kuja kama eneo gumu kwenye ngozi ya titi.

➡️Lakini sio kila ngozi ngumu kwenye titi ni saratani, huweza kutokea hata wakati wa hedhi au kunyonyesha.

➡️Ni muhimu hali hii kwenye titi kuangaliwa na daktari ili kujihakikishia.
DALILI 2 - KISHIMO KWENYE TITI (Dimple)

➡️Uvimbe wa saratani huweza kuvuta ngozi na tishu za titi ndani na kusababisha kishimo.

➡️Kishimo ambacho hakiondoki huweza kuwa dalili ya uvimbe ndani za titi hivyo huitaji uchunguzi.
DALILI 3 - UKOKO KWENYE CHUCHU (Crusty)
➡️Hali ya ukoko kwenye chuchu mara nyingi huwa sio tatizo kubwa, vilevile huweza kuwa dalili ya ugonjwa wa Paget.

➡️Seli za saratani ya ziwa huweza kuishi katika chuchu na kusababisha hali ya ukoko hasa wekundu ambao hautoki.
DALILI 4 - WEKUNDU KATIKA ZIWA
➡️Wekundu na ziwa kupata joto mara nyingi ni dalili ya maambukizi kwenye ziwa (mastitis) hasa wanaonyonyesha.

➡️Lakini kama matibabu hayasaidii; wekundu kwenye maeneo ya ziwa huweza kuwa dalili ya aina ya saratani (inflammatory breast cancer).
DALILI 5 - CHUCHU KUTOA MAJIMAJI
➡️Chuchu zinapoanza kutoa majimaji yanayotoka katika kipindi usipotarajia mfano: Huna maambukizi, huna ujauzito wala hunyonyeshi ni muhimu hiyo hali ikaangaliwa na daktari.
DALILI 6 - KIDONDA/VIDONDA KWENYE TITI

➡️Saratani ya matiti huweza kusababisha kidonda kwenye titi.

➡️Mara nyingi kidonda hiki huambatana na uvimbe mgumu ndani ya titi.

➡️Kadri muda unavyokwenda kidonda hiki huweza kuanza kutoa harufu.
DALILI 7 - UVIMBE/KIVIMBE KWENYE TITI

➡️Uvimbe mlaini kwenye ziwa huweza sababishwa na changamoto mbalimbali ambazo sio saratani.

➡️Lakini uvimbe ambao ni mgumu, pia haujongei ndani ya ziwa huweza kuwa saratani.

Ni muhimu kila uvimbe kuangaliwa na daktari.
DALILI 8 - CHUCHU KUINGIA NDANI

➡️Mabadiriko kwenye umbo la chuchu kama chuchu kuingia dani huweza kuwa dalili ya saratani.

➡️Uvimbe wa saratani ukiwa unakua ndani ya titi huvuta chuchu kuelekea kwake.
DALILI 9 - MSHIPA MPYA UNAOKUA KWENYE TITI

➡️Mara nyingi mtu anaponenepa au kunyonyesha matiti hupata mishipa ya damu inayoonekana kwenye ngozi.

➡️Lakini katika hali ambayo ni nadra sana; mshipa mpya kwenye ngozi ya titi huweza kuwa dalili ya saratani ya titi.
DALILI 10 - TITI KUBADILIKA UMBO AU UKUBWA
➡️Kwa kawaida ujauzito, unyonyeshaji au hedhi huja na mabadiriko ya umbo/ukubwa wa maziwa.

➡️Lakini iwapo titi moja bila kutarajia linapovimba, kubadiri umbo au kuanguka ni dalili inayohitaji uchunguzi.
DALILI 11 - NGOZI YA TITI KUWA KAMA GANDA LA CHUNGWA

➡️Ngozi ya titi mara nyingi ni laini.

➡️Inapotokea ngozi ya titi kuanza kupata mwonekano kama ganda ya chungwa huweza kuwa dalili ya saratani hasa aina inayoitwa "inflammatory breast cancer".
MUHIMU

⚠️Iwapo utagundua au utaona badiriko lolote kwenye matiti/titi ni muhimu kutopuuzia.

✍️Nenda Hospitali

✅Daktari atachukua historia yako na kukupima pia kuna vipimo muhimu kwenye uchunguzi kama mammogram utafanyiwa.
Saratani ya matiti inatibika, chukua hatua mapema, itambue na wahi kupata ushauri wa kitaalamu.

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Dr. Norman Jonas

Dr. Norman Jonas Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @NormanJonasMD

Oct 1
#AfyaSwahili | MAMBO MUHIMU KUFAHAMU KUHUSU UGONJWA WA EBOLA.

--> Uzi huu ni muhimu kutokana na kuwepo kwa mlipuko wa Ebola katika nchi jirani na elimu ya msingi ni muhimu sana.
➡️Ebola ni ugonjwa unaotokana na maambukizi vya virusi.

➡️Ugonjwa huu ni miongoni mwa magonjwa ya mlipuko yajulikanayo kama homa za virusi ambazo huambatana kutokwa damu sehemu mbalimbali za mwili (Viral haemorrhagic fevers).
➡️Ebola ni ugonjwa hatari sana.

➡️Kwa wastani husababisha vifo kwa wastani wa nusu wa watu wote waliougua.

➡️Uwezo wa kusababisha vifo hutofautiana kati ya mlipuko na mlipuko kwa wastani vifo huwa 20% hadi 90% ya wagonjwa.
Read 9 tweets
Nov 14, 2021
#DondooZaDaktari | Leo ni siku ya ugonjwa wa KISUKARI duniani #WorldDiabetesDay

➡️Siku maalumu ambayo wanajamii tunaelimishana kuhusu tatizo hili la kiafya.

➡️Tatizo hili linaongezeka na moja ya kisababishi kikuu cha magonjwa ya figo,moyo, upofu na ulemavu wa kupoteza viungo.
#KISUKARI NI NINI?

➡️Kisukari ni ugonjwa wa kudumu ambao hutokea pale kiwango cha sukari (glukosi) katika damu
kipo juu zaidi kutokana na kukosekana au mwili kushindwa kutumia homoni ya insulini

➡️Kiwango cha glukosi kikiwa juu kwa muda mrefu, husababisha madhara katika mwili
➡️Unapokula chakula, mfumo wako wa kumeng’enya hukichakata na kutengeneza glukosi.

➡️Glukosi inapoingia kwenye damu, husababisha kongosho lako kutoa homoni inayoitwa insulini.

➡️Insulini huzunguka mwilini na kuwezesha seli kupata glukosi ili kuitumia kuleta nguvu mwilini.
Read 17 tweets
Oct 29, 2021
#DondooZaDaktari | Leo ni siku ya #KIHARUSI #WorldStrokeDay

➡️Tatizo la dharura la kiafya ambalo ni moja ya magonjwa yanayoongoza kusababisha vifo.

➡️Mitindo ya maisha na Lishe ni vitu vinavyochangia wagonjwa wanaopata stroke kuongezeka

➡️Kiharusi huacha ulemavu au kifo
➡️KIHARUSI hutokea pale seli za ubongo 🧠 zinapokufa kutokana kuziba au kupasuka kwa mishipa ya damu kwenye ubongo hivyo kukosa hewa ya oksijeni na virutubisho.

➡️Kiharusi kikihusisha mshipa wa mkubwa wa damu kwa wastani mgonjwa hupoteza seli za ubongo (neuroni 1.9) kila dakika.
KUNA AINA KUU MBILI ZA KIHARUSIBrain

1️⃣Kiharusi kinachotokana na kuziba kwa mishipa ya damu ya damu ya ubongo

2️⃣Kiharusi kinachotokana na kupasuka kwa mishipa ya damu ya ubongo

🗒️80% ya watu wanaopata kiharusi hutokana na kuziba kwa mishipa ya damu kwenye ubongo.
Read 12 tweets
Oct 28, 2021
#DondooZaDaktari | #USUGU WA #DAWA

➡️ #Antibiotiki ni dawa zinazotumika kutibu maambukizi ya bakteria.

➡️Usugu wa antibiotiki hutokea pale bakteria wanapotengeneza usugu dhidi ya aina flani ya dawa.

➡️USUGU hufanya dawa kushindwa kufanya kazi

#AntimicrobialResistance
Matumizi holela ya dawa aina ya antibiotiki huchangia usugu wa dawa kutokea.

Bakteria wanapopata usugu husababisha
➡️Kutokupona ugonjwa hata baada ya kutumia antibiotiki ambazo zimekuwa zikitibu ugonjwa huo
➡️Kuongezeka kwa gharama za matibabu
➡️Kifo
Unatengeneza tatizo usugu wa dawa iwapo
➡️Humalizi dawa ulizoandikiwa na daktari
➡️Unatumia dawa zisizo na ubora/feki
➡️tumia dawa zilizoisha muda wake wa matumizi
➡️Unakula nyama, maziwa, mayai au damu yenye masalia ya antibiotiki kutoka kwa mifugo iliyotibiwa
Read 4 tweets
Oct 27, 2021
#DondooZaDaktari | Ugonjwa wa kisukari unaongezeka kwa kasi hata katika nchi zetu maskini.

✍️Kisukari hutokana na mwili kushindwa kutumia glukosi (sukari)

➡️Kisukari ndio sababu kuu ya:
- Kiharusi
- Upofu
- Ugonjwa wa kudumu wa figo
- Shambulio la moyo
- Watu kukatwa miguu Image
➡️Kwa mwaka 2019, takribani vifo millioni 1.5 Duniani vilichangiwa moja kwa moja na tatizo hili la kisukari.

➡️ Kuanzia mwaka 2000 hadi 2016, kuna ongezeko la 5% la vifo katika umri mdogo (premature death) kutokana na kisukari. Image
➡️ Mlo sahihi
➡️ Mazoezi ya Mwili
➡️ Kudhibiti Uzito
➡️ Kuepuka sigara na pombe

Ni baadhi ya mitindo ya maisha inayoweza kusaidia kuzuia kisukari au kupunguza athari ya kisukari aina ya pili.
Read 4 tweets
Jul 7, 2021
#CORONA --- #UVIKO19 UZI 👉 Je dalili kwa sasa ni zipi? Zimebadirika ? Picha ya ugonjwa ukiambukizwa ni ipi kwa sasa?
DALILI HUTOFAUTIANA KULINGANA UKALI WA UGONJWA?
✍️Tafiti kuhusu makali ya ugonjwa wa Korona-19 (UVIKO-19) yameonyesha makundi 3 ya wagonjwa

1. Ugonjwa usio mkali (81 kati ya 100)

2. Ugonjwa mkali maana mtu anahitaji oksijeni au 50% limeshambuliwa na ugonjwa (14 kati ya 100)
3. Ugonjwa mahututi maana mfumo wa upumuaji kushindwa kufanya kazi au ogani muhimu kama moyo, figo , ini kufeli

✍️HATARI YA KIFO: Kwa wastani vifo hutokea kwa asilimia 2.3 ya watu waliopata maambukizi kumaanisha asilimia wanopata maambukizi ya Corona 97.7 hupona
Read 18 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Don't want to be a Premium member but still want to support us?

Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal

Or Donate anonymously using crypto!

Ethereum

0xfe58350B80634f60Fa6Dc149a72b4DFbc17D341E copy

Bitcoin

3ATGMxNzCUFzxpMCHL5sWSt4DVtS8UqXpi copy

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!

:(