NAMNA YA KUTENGENEZA PESA MTANDAONI

Kutoka michezo ya Betting mpaka uuzaji wa nguo katika mitandao. Kuna namna nyingi sana za kutengeneza pesa mtandaoni, nyingine zina ahadi ya kukupa utajiri mkubwa ndani ya muda mfupi., lakini je, ni kweli zinafanya kazi? 👇

#ElimikaWikiendi
Jibu: Sio siku zote.
Je, Utatengeneza pesa ukifata njia hizo?
Jibu: Labda, maana ni kitu kimekaa kimtego sana. Inawezekana kabisa kwamba ile kazi yako inayokupa mshahara kila mwisho wa mwezi ikakupa pesa zaidi ya hizi njia za mitandaoni au kinyume chake

#ElimikaWikiendi
Ukweli ni kwamba kuna njia za kweli zinazofanya kazi na zinazowapa watu pesa kupitia mitandao. Kuna Freelancer(Wafanyakazi huru), wajasiriamali wadogo wadogo, waandishi, Walimu, Wahasibu, Wanasheria, N.K hutumia mitandao kupata kipato

#ElimikaWikiendi
Kuna njia nyingi unaweza kuzitumia ukakaa nyumbani au ofisini kwako ukiwa na simu/computer yako na ukaanza kuingiza pesa kupitia mitandao.

Leo ngoja tuangalie njia za kweli ambazo zinaweza kukupatia kipato mtandaoni

#ElimikaWikiendi
1.Mfanyakazi Huru (Freelancing)

Njia rahisi zaidi ya kuingiza kipato mtandaoni ni kupitia freelancing, Hapa wengi hutumia hobby/fani zao au ile kazi ilikuwa inakulipa mshahara kama njia ya kupata kipato unaweza kuifanya mtandaoni

#ElimikaWikiendi
Mfano wewe ni mwandishi, graphics designer, mwalimu, developer, mkalimani N.K, unaweza kuyatangaza haya maarifa mtandaoni na yakaanza kukupa kipato bila ya wewe kuwepo ofisini.

Kuna watu mtandaoni wapo tayari kukulipa uwafanyie kazi bila ya wewe kuwa na ofisi

#ElimikaWikiendi
Ni, wapi unaweza kuuza maarifa uliyonayo?
Kuna tovuti kadhaa unaweza kuuza maarifa yako, tukianza na moja ya nyumbani inaitwa gigspacetz.co.tz

Nyingine za huko nje ni

fiverr.com
freelancer.com
upwork.com

#ElimikaWikiendi
2.Kuwa Influencer

Influencer ni mtu ambaye ametengeneza jina lake kama brand na kulitumia kama njia ya kufanya matangazo ya watu binafsi au makampuni makubwa.

Cristiano Ronaldo ni influencer anayelipwa pesa nyingi sana kwa kila post moja ya instagram/Twitter

#ElimikaWikiendi
Kuwa influencer ni lazima ujenge jina lako kuwa brand, uwe na followers wa kweli wanao like au kucomment kwenye post zako.

Sio kuwa na followers 10k lakini post yako yenye wiki nzima ina 3 likes na 0 comments.

#ElimikaWikiendi
Kutengeneza pesa kama influencer unawezalipwa kwa post, affiliate links, kuwa wakala wa bidhaa za kampuni kubwa na wakati mwingine unaweza lipwa ili tu sura yako ionekane katika hafla fulani.

Sehemu rahisi za kufanya influencing ni Facebook, Twitter, Instagram na YouTube
3.Tengeneza pesa kwa Affiliate marketing.

Affiliate marketing ni utangazaji wa bidhaa ya brand fulani kwa kutumia link ya pekee wanayokupa. Link hii itatumika kuonesha ni watu wangapi wamenunua bidhaa ya kampuni hiyo kupitia tangazo uliloweka wewe.

#ElimikaWikiendi
Mfano, Leo Bohny Chengula akanipa link nitangaze simu zake, kwa makubaliano ya kwamba nachukua 10% ya kila mauzo ya hiyo simu, Mteja atakapo nunua hiyo simu kupitia ile link niliyopost mimi, Mimi nitachukua 10% ya alicholipia na Bohny atachukua yote inayobaki

#ElimikaWikiendi
Ukitaka kufanikiwa vizuri katika affiliate marketing, kitu inabidi ujue ni uandishi wa matangazo na kuwa muuzaji mzuri [ COPYWRITING SKILLS ] pia ni vyema ukafanya affiliate marketing kwa vile vitu unapenda itakuleta kipato zaidi,

#ElimikaWikiendi
4.Anza kufanya Dropshipping na Dropservice.

Dropshipping & Dropservice ni uuzaji wa bidhaa au maarifa kama mtu wa kati (Dalali). Mf Leo najua kwamba @HabariTech ni mtengenezaji wa Mobile apps lakini mimi siwezi. Nitakachofanya najitangaza mimi kama mtengenezaji wa Mobile Apps
Mteja akipatikana app iliyotakiwa kutengenezwa kwa Tsh. 5 mil nitasema natengeneza kwa Tsh. 6 mil. Nachukua Tsh. 5 mil nampa @HabariTech anatengeneza hiyo app nampa mteja, mimi nina Tsh. 1 mil mfukoni. Hapo ni kila mtu ashinde mechi zake ( Huo ni mfano 😄 )

#ElimikaWikiendi
Dropshipping inahusika na uuzaji wa bidhaa wakati Dropservice ni uuzaji wa maarifa. Katika Dropshipping iskutishe kwamba bidhaa utazitoa wapi, Kumbuka wewe humiliki hizo bidhaa. Wewe umewapa wateja sehemu ya kununulia bidhaa

#ElimikaWikiendi
anayehangaika na kufanya packaging na usafirishaji ni yule muuzaji/mmiliki wa hizo bidhaa

Kwenye Dropservice hakikisha unajikita na vitu ambavyo unavielewa au una-idea navyo ili kuepuka hasara, unaweza kumwambia mtaje bei flani na ikawa ndogo kuliko bei halisi

#ElimikaWikiendi
5.Anzisha darasa mtandaoni.

Kuuza elimu uliyonayo ni njia moja wapo ya kukuingizia kipato mtandaoni. Wewe una elimu ya kutosha kuhusu somo fulani. Tengeneza kozi ya hicho unachokijua vizuri kisha uza kozi hiyo sehemu kama Udemy.com

#ElimikaWikiendi
au kama una website yako mwenyewe basi uza katika website yako, Ili uweze tengeneza kozi nzuri yafaa ukaangalia wengine wamefanya nini katika kozi zinazohusu hicho unataka kufanya itakusaidia kutengeneza kilichobora zaidi

#ElimikaWikiendi
6.Chapisha Ebooks.

Ebooks ni vitabu vya kielektroniki ambavyo unaweza kuvisoma kupitia simu au Computer yako, Unachohitaji kufanya ni kuandika kitabu na kukiweka katika muundo mzuri kabisa wa kuwa kitabu.

#ElimikaWikiendi
Watu wenapendelea kusoma katika simu zaidi ya kuwa na kitabu halisi mikononi. Kuna sehemu nyingi za kuuza vitabu kama Amazon.com, gumroad.com N.K

Uzuri wa Ebook huingii gharama yoyote ya kuchapisha au kumlipa mwandishi wako.

#ElimikaWikiendi
Sababu ni wewe mwenyewe unaandika na kuchapisha mtandaoni katika Platform yako pendwa.

7. Uza picha unazopiga kwa simu/camera yako au Graphic designs zako

Unaweza kuwa mbobezi katika upigaji wa picha au mtu tu unayependa kupiga picha kama hobby.

#ElimikaWikiendi
Unaweza tangaza kazi yako kupitia mitandao kama FB, instagram au twitter na watu wakapenda kazi zako wakakuomba uwafanyie kazi kwa malipo, kuna platforms unaweza weka picha zako na zikauzwa mfano wa platform ni foap.com au 99designs.com

#ElimikaWikiendi
8. Tengeneza Youtube channel

Kama wengine wanaweza pata kipato kupitia Youtube kwanini wewe ushindwe? Mtu anayelipwa zaidi na YouTube ni kijana mdogo anaitwa Ryan, anafanya reviews za toys za watoto. Kufikia 2018 channel yake ilimuingizia kiasi cha $22 mil

#ElimikaWikiendi
Katika youtube utaanza kulipwa pale utakapofikisha subscribers 1000

9: Unaweza kuuza designs au digital work kama NFT

NILITAMANI KUENDELEA ILA NIMEFIKIA LIMIT YA TWEETS KWENYE THREAD, TUTAKUA NA SEHEMU YA 2 🙏

AHSANTENI

#ElimikaWikiendi

Credit: @TOTTechs na @HabariTech

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with #TOTTechs 🇹🇿

#TOTTechs 🇹🇿 Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @TOTTechs

10 Jul
UZI:

RADAR NA MATUMIZI YAKE

RADAR
Radar ni kifupisho cha (Radio Detection and Ranging)
Ni mfumo ambao unatuma signal/ishara kwenye kitu (object) na kuchambuliwa kisha kurudisha majibu ya hicho kifaa kwa mfumo huo wa signal kupitia hewa 👇

#ElimikaWikiendi
Ili kugundua uwepo, mwelekeo, umbali, na kasi ya ndege, meli, na vitu vingine

Signal ni mawimbi (radio waves) ambayo hutumwa kwa kifaa kilicho kwenye coverage ya Radar/eneo Radar inapofika na kukichambua hicho kifaa na kurudisha majibu kwenye chanzo/muongozaji

#ElimikaWikiendi
Kwa hapa Tanzania radar zinatumika kwenye viwanja vya ndege, jeshini na kwenye Meli. Na radar zilizopo zimegawanyika katika makundi mawili: Primary na Secondary radar

Tunapozungumzia hizi primary radar tunamaanisha ni zile Radar ambazo

#ElimikaWikiendi
Read 18 tweets
22 Jun
DARASA LA CRYPTO:
SEASON 1: UZI/THREAD

MEME COINS/SHITCONS

Meme Coins au Shitcoins unaweza kuziita coins za majitaka au futuhi coins

Ni coins ambazo zimekua zikipendwa sana na watu wa Crypto kwa kuwa zinaweza kukupa faida hata mara 1000 ya mtaji wako kwa muda mfupi. 👇
Meme coins zimeundwa bila kuwa na matumizi yoyote muhimu kasoro kiki inayotokana na Jina la hiyo coin.

Katika msimu huu wa Crypto, shitcoins zimekua zikipatikana sana katika Blockchain inayoitwa Binance Smart Chain (BSC) kupitia website inayoitwa Pancakeswap
na kununua inabidi uwe na salio la coin ya BSC inayoitwa BNB na iwe ndani App ya TrustWallet...utatumia adress ya hiyo coin yako ili kuinunua

Kwa kawaida tumezoea Coin inakua na project fulani ili watu wawekeze.
Sasa hizi MemeCoins hazina project yoyote zaidi ya kupigiwa Kiki
Read 19 tweets
1 Jan
APPLE

Mwaka 2021 unatabiriwa kuwa na mapinduzi ya Tekinolojia, Apple wao wamejipanga kufanya yafuatayo

UZI

◾️Apple silicon iMac

Apple wanakuja na iMac ambayo itakuwa na Apple silicon chip, kama walivyofanya kwenye MacBook, itakuwa na16 high-power cores& 4 efficiency cores ImageImage
◾️AirPods

2021 Apple wanategemea kutoa third-generation AirPods ambayo itakuwa na replaceable silicone air tips, pia wataboresha wireless chip na battery life Image
◾️iPad Pro

Apple wanakuja na 12.9 inch iPad Pro ambayo itakuwa na LED display, hii Min-LED Technology itakuwa na wide color gamut performance, high contrast and HDR, and local dimming, pia iPad Pro itakuwa na 5G connection ikisapotiwa na A14X chip kama ilivyo kwenye M1 Macs Image
Read 13 tweets
19 Dec 20
UZI

SOCIAL ENGINEERING
[ utumiaji wa madhaifu ya Mwanadamu kufanya wizi]

◾️Social engineering huchukua faida ya kitu dhaifu kabisa katika ulinzi wa taarifa za kila aina ya taasisi ambacho ni MTU

Social engineering ni "PEOPLE HACKING" na inahusisha 👇

#ElimikaWikiendi Image
Madhaifu ambayo binadamu tunayajenga sisi kwa sisi na kuweza kuyatumia hayo madhaifu kupata taarifa ambazo hutumika kwa faida binafsi

◾️Social engineering ni moja ya wizi mgumu kufanyika, kwa Dunia ya sasa imekuwa ni vigumu sana mtu kumwamini mtu mgeni kwake

#ElimikaWikiendi Image
Kutokana na hali halisi ilivyo hata hivyo hii imekuwa hacking ngumu sana kuizuia kutokana na uaminifu tunaoujenga baina yetu

◾️Social engineering, typically yule malicious attacker/mwizi hujiweka kama mtu mwema sana ili kupata taarifa anazotaka

#ElimikaWikiendi Image
Read 25 tweets
27 Oct 20
TWITTER FOR VPN

◾️kumekuwa na sintofahamu baina yetu na kulazimika kutumia VPN ili kuweza kupata access ya twitter

◾️Hii inasababishwa na kitu kinaitwa OUTAGE kwa jina jingine ni DOWNTIME

◾️Twende na uzi uelewe inatokeaje na kwa nini unatumia VPN/TOR/PROXIES

Uzi mfupi
◾️Outage kwa jina jingine ni Downtime ambapo ni ukosefu wa huduma flani au network, Hii inakuwa imegawanyika kwa namna mbili

👉 Unplanned outage
👉 Planned outage

◾️Unplanned outage ni ukosefu wa huduma flani au network nzima kutokana na mambo kadhaa kama vile
✴️Kuingiliwa/kuzimwa kwa network/mawasiliano na attackers (wadukuzi) hii inaitwa DOS/DDOS [ Denial of services ] attack

✴️ Kufeli kwa Hardware au Software

✴️ Kuharibika kwa vifaa flani vinavyotoa huduma ya internet

◾️Planned outage ni ukosefu wa huduma au network
Read 7 tweets
24 Oct 20
iPhone 12 Pro Max VS Samsung Note 20 Ultra

◾️Hizi ni simu zinazotamba kwa sasa Duniani ikiwa ni matoleo mapya kwa Samsung na Apple

◾️Nakuletea ulinganifi wa hizi simu, hii ni kulingana na majarida mengi kama AndroidAuthority, CNet, GSMArena, Gadget360 n.k

Twende na uzi👇 Image
◾️Samsung Galaxy Note 20 Ultra ilitoka Aug 5 na iPhone 12 Pro Max ilitoka Oct 13 lakini hii bado ni Pre-order

◾️Kila kampuni inasifia simu yake kuwa ni bora zaidi Duniani kwa sasa kutokana na teknologia ya hali ya juu iliyotumika kwenye hizo simu

◾️Tuzichambue taratibu ImageImage
◾️DESIGN

👉 Simu zote zinamwonekano mzuri lakini kuna utofauti

◾️Samsung Galaxy Note 20 ultra ni simu yenye kuonekana vizuri sana, wamechukua designing ya matoleo yote ya Note series wakaleta hii Note 20 ultra, dimensions 168.4mm/urefu 77.2/upana 8.1/angle na uzito ni 208g Image
Read 18 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!

:(