ZIMWI TULIJUALO: USO KWA USO NA CIA NDANI YA AFRIKA MASHARIKI

PART 2

Sasa basi,

Wale maaskari wawili ambao walifika Upanga nyumbani kwa Mohammed al-Asad sio tu kwamba walikuwa wamevalia kiraia tu, bali pia walifika wakiwa na gari yenye plate number za kiraia pia.

Kwa hiyo... Image
wakamwambia al-Asad kwamba wanahitaji kwenda naye kituo cha polisi kwa ajili ya mahojiani mafupi.

Kama ilivyo kawaida al-Asad akawauliza mahojiano hayo yahusu nini haswa? Polisi wakamjibu kwamba atafahamu huko huko kituoni akifika
Bila hiyana al-Asad akaaga familia yake na kisha
akaingia kwenye gari ambalo wale askari waliwasili nalo na kisha wakaondoka.
Gari ilipowashwa iliendeshwa mpaka kufika uwanja wa ndege Terminal 1 kwenye hangar ya kampuni ya Tanzania Air Services (Sio Air Tanzania.. hii ni kampuni binafsi ambayo bado ingalipo hata sasa nchini...
hawa wenyewe wanafanya biashara ya kutoa huduma ya usafiri wa anga kwa charted na private planes. Kwa mfano hata sasa hivi ukienda pale uwanja wa ndege Terminal 1 wana karakana yao. Hii ndio kampuni ya kwanza nchini kupewa kibali cha kufanya service ndege za Cessna).

Kwa hiyo..
ile gari ikafika mpaka hapo kwenye hangar ya Tanzania Air Services.
Walipofika wakamkabidhi al-Asad kwa wazungu wawili ambao walikuwata hapo wanawasubiri.

Wale wazungu wakamtia pingu al-Asad na kumveka tambara jeusi usoni ili asiwe kuona na kisha kumpakia kwenye ndege ndogo aina Image
ya Cessna F406 Caravan II, ambayo mkiani ina namba ya usajili 5H-TZE mali ya kampuni ya Tanzania Air Services Ltd.

Ile ndege ikaruka moja kwa moja toka hapa Dar es Salaam mpaka nchini Djibouti kwenye mji unaoitwa Ambouli ambako vikosi vya Navy vya Marekani wana kambi ya kudumu..
ya kijeshi inayoitwa Camp Lemonnier (hii ndio kambi pekee ya kudumu ya Marekani hapa barani Afrika. Kambi hii pia inafanya kazi kama makao makui ya U.S. Africa Command (USAFRICOM)).

Ndani ya kambi hii pia kuna 'black site' maarufu ya shirika la Ujasusi la CIA ambayo wanaitumia.. Image
kama jela ya siri kuwashikilia mateka wao muhimu ambao hawataki wajulikane kwamba wamewakamata.

Sasa huyu Asad ndio alipotolewa hapa Dar akapelekwa kwenye hiyo black site ya CIA ndani ya Camp Lemonnier nchini Djibouti

Kwa ufupi sana labda nimueleze huyu Asad.

Huyu somo ni raia
wa Yemen ambaye alikuwa ameishi hapa nchini kwetu kwa muda wa miaka 10.
Huyu bwana kwa muda huu ambao alikuwa ameishi hapa nchini alikuwa amefanikiwa kugushi cheti cha kuzaliwa kuonyesha kwamba ni mzaliwa wa hapa tz na hivyo alikuwa na hati ya kusafiria ya Kitanzania japo kwa..
uhalisia hakuwa raia wa Tanzania.

Sasa,

Masaa kadhaa baada ya kufikishwa hapo Camp Lemonnier, maafisa wengine wawili wa CIA walifika kwenye selo ya siri ndani ya kambi ambayo alikuwa anashikiliwa.

Kwa mujibub wa al-Asad mwenyewe kwa maelezo ambayo miaka kadhaa baadae alikuja.. Image
kuwaambia wajumbe wa Kamisheni ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Afrika aliwaelezea watu wale wawili waliokuja kwenye selo yake kwamba mmoja alikuwa ni mwanamama halfcast wa kizungu na kiafrika akiwa ameambatana na mwanaume wa Kizungu ambao wote walivalia kiraia

Maafisa hao wawili
wa CIA wakaanza kumuhoji.

Swali pekee ambalo walimuuliza Asad ni uhusika wake kwenye shirika linaloitwa Al-Haramain Foundation.

Hapo nieleze kidogo,

Huyu Asad shughuli yake aliyokuwa anaifanya hapa Dar alikuwa ni muhasibu wa hilo shirika linaloitwa Al-Haramain Foundation ambao
walikuwa na ofisi zao mtaa wa Kisutu.

Shirika hili la Kiislamu lilikuwa limejikita kwenye kutoa misaada ya kiutu kama vile kujenga vituo vya watoto yatima, kusadia kulipia vijana gharama za masomo, kusambaza bure vitabu vya dini na pia kuwachangia gharama watu wanaokwenda kuhiji
Shirika hili makao makuu yake yalikuwa yako nchini Saudi Arabia na kwa hapa Afrika lilikuwa na ofisi kwenye nchi nne tu, Ethiopia, Somalia, Kenya na hapa kwetu Tanzania.

Na kwa hapa Tanzania huyu al-Asad ambaye muda huu ameshikiliwa kwenye black site ya CIA nchini Djibouti..
alikuwa ndiye muhasibu.

Maafisa hao wa CIA wakamtaka aeleze nukta kwa nukta kile ambacho Asad anakifanya ndani ya shirika la Al-Haramain

Leo nimechelewa kidogo kuweka hii Part 2 kutokana na majukumu

Kesho usikose Part 3, Nisaidie ku-retweet

Habib B Anga
To Infinity and Beyond

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with Habibu B. Anga

Habibu B. Anga Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @habibu_anga

11 Apr
MTANZANIA #1: JASUSI WA KUKODI, UJASUSI WA BIASHARA

Thread..

Si rahisi kuwa mahususi sana ni mwaka gani, lakini tunakadiria kwamba katikati ya miaka ya tisini hivi Mtanzania ambaye kwa sasa nimtaje kwa jina lake moja tu la Matiko aliondoka jiji Dar kwenda nchini Afrika Kusini Image
Kwa ajili ya kutafuta maisha. Lakini tofauti na Watanzania wengi wanaozamia SA ambako wakifika uanza kwa kufanya shughuli za hali ya chini, ilikuwa tofauti kabisa na bwana Matiko ambaye aliingia SA akiwa na mtaji wa kuridhisha kutokana na fedha ambazo alizipata toka kwenye mauzo
ya sehemu ya shamba lake la karibia Ekari 300 zilizoko kijiji cha Ghesaria Wilayani Serengeti.

Matiko akatumia mtaji huo akiwa hapo SA kuanzisha biashara ndogo ndogo
Moja ya biashara aliyoanzisha ambayo ilipanda mbegu ya kumbadilisha Matiko na kumfanya aingie kwenye ulimwengu wa
Read 25 tweets
5 Apr
Kuna uzi niliandika hapa Mwezi March kuhusu dhana nzima ya Ulinzi wa viongozi wa juu.
Nikasisitiza sana kwamba sula la ulinzi wao sio tu kulinda wasidhuriwe kimwili bali pia kulinda hadhi zao, heshima zao na siri zao.

Kitimbwi ambacho kimetokea leo cha Rais wa nchi

Thread👇👇 Image
Kuteua na kufukuza Mkurugenzi wa TPDC ndani ya masaa machache kabisa... ni failure kubwa ya kitengo cha intelijensia ya nchi ambao wana jukumu la kulinda hadhi na heshima ya Rais.
Mtu yule aliyeteuliwa huku akionekana kwamba hana sifa kabisa ya kushika wadhifa ule, ina reflect..
ombwe la weledi ambalo linaikumba idara hii adhimu ya ujasusi.

Mhe. Rais @SuluhuSamia ambaye watu wametokea kuwa na imani naye sana, tukio la leo kwa kiwango fulani limetia doa hadhi yake na kuzua maswali mengi sana

Kwamba, kosa la dhahiri namna ile limetokeaje?
Intelijensia ya
Read 18 tweets
2 Apr
ZIMWI TULIJUALO: USO KWA USO NA CIA NDANI YA AFRIKA MASHARIKI

PART 5 (HITIMISHO)

Nikiwa nahitimisha ni vyema kusisitiza kwamba, kikosi hiki cha makomando wa Kenya ambacho kinaendeshwa kwa amri ya CIA na NIS (Idara ya Ujasusi Kenya) kwa sasa kimegawanywa kwenye vitengo viwili.. Image
Kitengo cha kwanza ndio ile Rendition Operations Team; hawa wanahusika sana kama target anatakiwa kukamatwa akiwa hai

Alafu siku hizi kuna RRT (Rapid Response Team) hawa wanatumika zaidi kama target anatakiwa kuwaneutralized (kuuwawa) au kuhusika kuokoa mateka kama watekaji wana
mafungamano na vikundi vya kigaidi na si lazima kuwakamata wakiwa hai.

Sasa nieleze baadhi ya Oparesheni ambazo makomando hawa wa Kenya na CIA wamewahi kuzifanya.

1. Kuuwawa kwa Sheikh Aboud Rogo

- Sheikh Aboud Rogo ni moja ya watu maarufu sana kwenye masuala ya dini kuwahi...
Read 25 tweets
1 Apr
ZIMWI TULIJUALO: USO KWA USO NA CIA NDANI YA AFRIKA MASHARIKI

PART 4

Ile taarifa ambayo Asad aliwapatia ilikuwa ya maana sana kwa CIA.

Mpaka muda huu ambapo Asad alikuwa anahojiwa (kumbuka hiyo ni mwaka Oct 2003) huyo "bwana somba" Odeh tayari alikuwa ameshakamatwa Image
na yuko gerezani Guatanamo Bay (alikamatwa tangu mwaka 1998).

Taarifa hii ya Asad iliwapa CIA kitu kimoja muhimu sana.. walithibitisha intelijensia yao kuhusu shirika la al-Haramain kutumiwa na al-Qaida kusambaza fedha ulimwenguni kwa watu wao.
Ushahidi huu ulitumiwa na Marekani
kushawishi Umoja wa Mataifa kulipiga marufuku shirika hilo na mpaka leo hii ninavyoandika shirika hilo ofisi zake zote ulimwenguni zimefungwa

Lakini hicho sicho ninachotaka kuandika
Ninachotaka kuandika ni namna ambavyo ile confirmation ya Asad iliwasaidia CIA kuanza kunusa kila
Read 16 tweets
1 Apr
ZIMWI TULIJUALO: USO KWA USO NA CIA NDANI YA AFRIKA MASHARIKI

PART 3

Mara ya mwisho nikasema kwamba, maafisa wawili wa CIA walifika kwenye jela ya siri ya shirika hilo la Ujasusi iliyopo ndani ya kambi ya Kijeshi ya Camp Lemonnier nchini Djibouti ambako "Mtanzania" al-Asad.. Image
alikuwa anashikiliwa.

Maafisa hawa wa CIA swali pekee ambalo walikuwa wanamuhoji Asad ni kuhusu shughuli zake ndani ya shirika la Kiislamu la al-Haramain ambalo yeye alikuwa kama muhasibu hapa Tanzania

Kwa muda wa siku tatu nzima, Asad alikuwa akihojiwa kwa mtindo ambao wenyewe
CIA huita "mbinu zilizoboreshwa" (enhanced techiques) ambazo kimsingi ni mateso kama vile water boarding, sleep depravation, light depravation.

Niweke nyama hapo kuhusu hili shirika la al-Haramain ambalo CIA walikuwa wakimuhoji Asad kuhusu.

Shirika hili la misaada la Kiislamu.. Image
Read 26 tweets
28 Mar
ZIMWI TULIJUALO: USO KWA USO NA CIA NDANI YA AFRIKA MASHARIKI

Thread..

Kwa sasa, eneo letu la Afrika Mashariki limeguka kuwa moja ya eneo muhimu sana la kimkakati kiulinzi kwa nchi ya Marekani.

Leo nataka nikusimulie mkasa halisi wa namna gani shirika la Ujasusi la Marekani...
CIA linaendesha shughuli zake kuanzia hapa nchini kwetu Tanzania pamoja na nchi zote zingine za Afrika Mashariki.
Nataka nikusimulie mkasa wa kusisimua ili tuelewe vyema namna gani Afrika Mashariki kwa sasa imegeuka uwanja wa ushushushu wa Kimataifa kati ya Marekani na adui zake.
Ukimaliza kusoma uzi huu, utaelewa kwa nini sio kila "mtalii" umuonae ni mtalii tu kaja kushangaa swala pale Mikumi

Namna hii,

Siku fulani hivi ya tarehe 7 mwezi June mwaka 2011, kuna vijana watatu walikuwa wanasafiri kwa gari binafsi toka pwani ya Somalia kwenye mji unaitwa...
Read 25 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!