๐™‰๐™…๐™„๐˜ผ 9 ๐˜ฝ๐™Š๐™๐˜ผ ๐™•๐™„๐™๐˜ผ๐™†๐˜ผ๐™•๐™Š๐™†๐™๐™๐˜ผ๐™‰๐™”๐˜ผ ๐™๐˜ผ๐™‰๐™•๐™€ ๐™…๐˜ผ๐™ˆ๐˜ฝ๐™Š ๐™‰๐˜ผ ๐™๐™๐˜ผ๐™‰๐™„๐™†๐™„๐™’๐™€ ๐™†๐˜ผ๐™๐™„๐™†๐˜ผ ๐™ˆ๐˜ผ๐™„๐™Ž๐™ƒ๐˜ผ ๐™”๐˜ผ๐™†๐™Š. #๐™€๐™ก๐™ž๐™ข๐™ž๐™ ๐™–๐™’๐™ž๐™ ๐™ž๐™š๐™ฃ๐™™๐™ž - ๐™๐™๐™ง๐™š๐™–๐™™ (๐™๐™•๐™„)
Kila siku tunajishughulisha ili tutimize malengo yetu. Katika maisha kuna watu ambao wanafanikiwa katika mambo yao na kuna watu ambao hawafanikiwi. Tunajishughulisha kila siku kuyatimiza malengo hayo. Malengo yanaweza yakawa ni maswala ya Elimu, Kazi, Biashara, Uongozi nk.
Tafiti zinaonyesha ni watu wachache sana wanaotimiza malengo yao duniani kote, inawezekana ukawa miongoni mwa watu ambao hawajafanikiwa kutimiza malengo yao. Zifuatazo ni njia 9 bora zitakazokufanya ufanikiwe katika maisha yako.
1. ๐–๐ž๐ค๐š ๐Œ๐š๐ฅ๐ž๐ง๐ ๐จ. Malengo ni dira, ni kitu pekee kinachokuonyesha unahitaji kutimiza nini. Huwezi kufanikiwa wala kushidwa kama hujui unahitaji nini. Kuna msemo unasema โ€œHuwezi potea kama hujui unapokwendaโ€ Malengo ni kipimo cha kushinda au kushindwa katika maisha yako.
Jiwekee malengo ya siku, wiki, mwezi, miezi mitatu, miezi sita, mwaka au zaidi ya mwaka. Unahitaji ujue unahitaji nini na kwa muda gani. Kwa mfano unaweza kupanga kutaka kuwa na elimu ya kiwango fulani, kua kiongozi katika ngazi fulani au kumiliki biashara.
Malengo hayo yaambatane na muda maalumu, kwasababu kama yasipokua na muda unaweza ukajikuta unatumia miaka 20 kununua Baiskel na ukajiona kua umefanikiwa, Ni kweli utakua umefanikiwa kununua baiskeli ila muda uliotumia ni mwingi kuliko uzito wa lengo lenyewe.
2. ๐“๐ž๐ง๐ ๐ž๐ง๐ž๐ณ๐š ๐ฆ๐ฉ๐š๐ง๐ ๐จ ๐ฆ๐ค๐š๐ค๐š๐ญ๐ข ๐ฐ๐š ๐ค๐ฎ๐ญ๐ข๐ฆ๐ข๐ณ๐š ๐ฆ๐š๐ฅ๐ž๐ง๐ ๐จ ๐ฒ๐š๐ค๐จ. Baada ya kujua unataka kutimiza nini unatakiwa upange ni jinsi gani unakwenda kutimiza lengo lako. Mpango mkakati ni njia na mbinu mbalimbali utakazozitumia kutimiza malengo yako.
3. ๐ƒ๐ก๐š๐ฆ๐ข๐ซ๐ข๐š ๐ค๐ฎ๐ญ๐ข๐ฆ๐ข๐ณ๐š ๐ฆ๐š๐ฅ๐ž๐ง๐ ๐จ ๐ฒ๐š๐ค๐จ.Dhamira itakufanya upigane kufa kupona ili jambo lako litimie. Moja ya sababu inayofanya watu washidwe kutimiza malengo yao ni kukosa dhamira ya kutimiza malengo yao
4. ๐Š๐ฎ๐ฐ๐š ๐ญ๐š๐ฒ๐š๐ซ๐ข ๐ค๐ฎ๐ฃ๐ข๐ญ๐จ๐š. Kujitoa kunahitaji moyo. Uwe tayari kujitoa kuyaacha mambo uliyoyazoea au unayopendelea kuyafanya na kuanza kufanya mambo yanayopelekea kutimiza malengo yako.
5. ๐Š๐ฎ๐ฐ๐š ๐ง๐š ๐ง๐ข๐๐ก๐š๐ฆ๐ฎ. Kila jambo linahitaji nidhamu. Nidhamu ni zana muhimu sana ya kutumia wakati wa kusaka mafanikio ya aina yoyote. Nidhamu maana yake nini katika kutafuta mafanikio? Ni kufata mipango na mikakati yote uliyojiwekea katika kutimiza malengo yako.
6. ๐”๐ฌ๐ข๐ค๐š๐ญ๐ž ๐ญ๐š๐ฆ๐š๐š. Katika safari ya mafanikio inakua na vikwazo vingi sana. Kama unaona unatimiza lengo ambalo halina vikwazo basi ujue hilo lengo si saizi yako. Lengo ambalo zuri na lenye tija linakua na vikwazo vingi sana tena kuna wakati unajihisi ata kulia.
7. ๐”๐ฌ๐ข๐›๐ฐ๐ž๐ญ๐ž๐ค๐ž na machache uliyoanza kuyatimiza. Katika safari ya mafanikio kuna kipindi utafika utaanza kuona matunda ya jitihada zako. Hapa wengi hukosea, watu wengi wakishaanza kuona matunda ya jitihada zao basi kama alikua akifanya sana kazi utakuta anaanza kuzembea.
Katika kipindi ambacho unatakiwa ukazane sana tena sana yaani uongeze juhudi mara mbili ni kipindi cha kuanza kuona matunda ya jitihada ulizoziweka juu ya jambo fulani.
8. ๐–๐ž๐ค๐š ๐›๐ข๐๐ข๐ข ๐ฌ๐š๐ง๐š. Dunia ya sasa ni dunia ya ushindani, kila unachokifanya unatakiwa ukifanye kwa ufanisi mkubwa sana. Kila kitu ni kushindana, ukifanya jambo kwa uvivu hautafanikiwa kamwe.
9. ๐‰๐ข๐ญ๐š๐ญ๐ก๐ข๐ฆ๐ข๐ง๐ข. Kila hatua unatakiwa uangalie ulipotoka, ulipo na unapokwenda katika kutimiza malengo. Hili litakusaidia kujua umahiri na udhaifu wako. Na hata kama utashidwa itakusaidia kujua ni kipi kilipelekea ushidwe na kuweza kijirekebisha katika mpango mwingine.
Naamini kupitia njia hizi basi utakua mtu tofauti Nakutakia mafanikio mema.

๐Œ๐ฐ๐š๐ค๐š ๐ก๐ฎ๐ฎ ๐ฎ๐ง๐š ๐ฆ๐š๐ฅ๐ž๐ง๐ ๐จ ๐ ๐š๐ง๐ข? ๐‘๐„๐“๐–๐„๐„๐“, ๐‹๐ˆ๐Š๐„ ๐ฆ๐š๐ซ๐š๐Ÿ๐ข๐ค๐ข ๐ณ๐š๐ค๐จ ๐ง๐š๐จ ๐ฐ๐š๐ฉ๐š๐ญ๐ž ๐ฆ๐š๐š๐ซ๐ข๐Ÿ๐š.
@threadreaderapp please unroll

โ€ข โ€ข โ€ข

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
ใ€€

Keep Current with Gillsant 5.5

Gillsant 5.5 Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @GillsaInt

26 Sep 20
๐‘ฐ๐‘ณ๐‘ฐ ๐‘พ๐‘จ๐’๐‘ถ ๐‘ณ๐‘จ๐‘ฒ๐‘ถ ๐‘ณ๐‘จ ๐‘ฉ๐‘ฐ๐‘จ๐‘บ๐‘ฏ๐‘จ๐‘น๐‘จ ๐‘ณ๐‘ฐ๐‘ญ๐‘จ๐‘ต๐‘ฐ๐‘ฒ๐‘ฐ๐‘พ๐‘ฌ ๐‘ฝ๐‘ฐ๐‘ป๐‘ผ ๐‘ฝ๐’€๐‘จ ๐‘ฒ๐‘ผ๐’๐‘ฐ๐‘ต๐‘ฎ๐‘จ๐‘ป๐‘ฐ๐‘จ: ๐‘ผ๐’๐‘ฐ ๐‘ท๐‘จ๐‘น๐‘ป 2
Vitu vingine vya kuzingatia wakati unakuja na wazo lako la biashara.
Yes unaweza fungua biashara kutokana na kitu unachokijua mfano Kinyozi ukafungua saluni yako au mpishi ukafungua restaurant yako. Kumbuka kwakua wewe ni mpishi mzuri sio kwamba utafahamu jinisi ya kuendesha restaurant yako vizuri. Kuna mambo mengi ya kuzingatia
Kama unataka biashara endelevu make sure huduma au bidhaa unayouza wateja wako watarudi kwako tena. Inabidi uwe na bidhaa au huduma ambayo wateja wataendelea kununua kwa muda mrefu. Mfano ni bora uwe na kampuni ya kusafisha swimming pool kuliko kua na kampuni ya ujenzi wa pool.
Read 19 tweets
26 Sep 20
๐‘ฑ๐‘ฐ๐‘ต๐‘บ๐‘ฐ ๐’€๐‘จ ๐‘ฒ๐‘ผ๐‘ฑ๐‘จ ๐‘ต๐‘จ ๐‘พ๐‘จ๐’๐‘ถ ๐’๐‘ผ๐‘น๐‘ฐ ๐‘ณ๐‘จ ๐‘ฉ๐‘ฐ๐‘จ๐‘บ๐‘ฏ๐‘จ๐‘น๐‘จ. Ili kuweza kufanikiwa kwenye biashara unahitaji kuwa na wazo zuri la biashara. Je unajua jinsi ya kupata wazo hilo zuri la biashara? ๐‘ผ๐’๐‘ฐ, ๐‘ท๐‘จ๐‘น๐‘ป 1
Watu wengi wamekuwa wakiniomba ushauri ni wazo gani zuri la biashara ambalo linaweza kuwapatia faida na mafanikio. Ukweli ni kwamba wazo ambalo ni bora kwa mtu fulani linaweza lisiwe bora kwako.
Moja ya sababu zinazofanya biashara nyingi kufa au kutokuendelea ni kuiga, yaani mtu akianza biashara leo baada ya muda unakuta watu wengine wameiga biashara ile ile, wanaifanya eneo lile lile na kwa mbinu zile zile. Hii ni njia rahisi sana ya kushindwa kwenye biashara.
Read 22 tweets
29 Aug 20
JINSI YA KUANZISHA BIASHARA UKIWA UMEAJIRIWA: Biashara yoyote iwe mpya au ya zamani ina changamoto zake especially kwenye mazingira yetu. 50% Ya biashara zote ndogo zinakufa katika mwaka wake wa kwanza kuanzishwa. UZI #ElimikaWikiendi
Mtandao wa Investopedia ulitoa sababu ya biashara ndogo kufa, 1. Mtaji Mdogo, 2. Uendeshaji Mbovu, 3. Mpangilio Mbovu wa Biashara na Bidhaa yako au huduma yako haihitajiki sokoni (Hakuna wateja wanahitaji bidhaa zako). Pamoja na sababu zingine nyingi.
Sasa kama tulivyoona hapo juu changamoto ni nyingi. Kabla ya kufikiria kuanzisha biashara ukiwa umeajiriwa inabidi ujipange. Kitu kimoja kikubwa ambacho Ajira itakusaidia kipindi unataka kuanzisha biashara ni MTAJI pamoja na muda wa kujipanga kabla ya kuanza biashara full time.
Read 16 tweets
8 Aug 20
NJIA (Business Models) 10 ZA KUPATA PESA ONLINE. UZI Nimeshindwa kupata kiswahili cha Business Model (Mtanisaidia) Kwa uzoefu wangu watu wengi wanapotaka kuanza kufanya biashara Online or Offline. Hua wanafikiria njia moja au Mbili. #GillMadini
Kununua Bidhaa kutoka sehemu fulani au Kutengeneza hio bidhaa na kuiuza dukani or ikizidi sana mtandaoni kupitia Instagram au Facebook wachache kwenye website. Leo nimewaletea Business Models zingine 10. Ambazo unaweza kutumia kupiga hela.
Tukirejea kwenye UZI nilioandika mara ya mwisho. Kama bado haujausoma tafadhali usome Halafu rudi kumalizia Uzi huu. Leo nitatoa mfano wa wazo moja la biashara mbalo unaweza tumia njia zaidi ya 10 (10 Business Models) tofauti kuweza kufanikisha kujipatia pesa.
Read 24 tweets
23 Jul 20
BIASHARA MTANDAONI: Kuna njia nyingi za kuanza kufanya biashara mtandaoni (Facebook, Twitter, Instagram). Watu wengi hua tunakwama ni wazo gani la biashara au bidhaa gani niuze itakua na wateja. Nimekuletea UZI huu ukusaidie njia fupi ya kupata bidhaa ya uhakika kuuza #GillMadini
Kuna njia 2 ambazo ntazielezea kwa ufupi. 1. Kama tayari ushafahamu ni bidhaa gani utaenda kuuza mtandaoni 2. Hufahamu bidhaa au huduma gani uchague na kuuza mtandaoni.
Last time niliongelea hili swala lakini leo pia ningependa kutoa msisitizo, Idea za bidhaa za kuuza zipo nyingi sana lakini kuna maeneo haya ukipata bidhaa zake unatoboa faster Afya, Urembo, Passion, Hobby, Interest, Activities, Self Improvement, Wealth and Money, fitness.
Read 42 tweets
11 Jul 20
"Namna Sahihi ya kuanzisha na kuendeleza biashara kwa mtaji mdogo mtandaoni." Nimejaribu kila naloweza kuandika points kwa kifupi ili hii topic iweze kueleweka lakini imeshindikana. Hivyo basi.. UZI (THREAD) #ElimikaWikiendi
Kutokana na uzoefu wangu biashara nyingi za mtandaoni hazifaikiwi kwa sababu zinaendeshwa kwa mazoea au kwa kubahatisha. Ukifuata mfumo wa jinsi ya kuanzisha biashara kwa usahihi huwezi kulalamika hakuna wateja au bidhaa hainunuliwi.
Hizi ni baadhi ya steps unatakiwa kuzifuta CUSTOMER RESEARCH, PRODUCT RESEARCH, MARKET RESEARCH, FINANCIALS, OPERATIONS, BRANDING, CONTENT CREATION (MARKETING), COPYWRITING, ONLINE ADVERTS, ONLINE SALES, ACCOUNT GROWTH, ALGORITHM, CUSTOMER CARE, BUSINESS FORMALIZATION
Read 21 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!