📡Part 2: Sim Cards zinaiwezesha vipi simu kufanya kazi?

Simu yako haina maana kama utashindwa kupiga/kupokea simu za kawaida au kutuma SMS.

Unapokuwa na simu utahitaji kuunganishwa na mtandao flani ili kupata huduma ya za simu.

#HabariTech
📡Unapochagua kusajili sim card ya mtandao uupendao unakuwa umesajili akaunti ambayo utakuwa unailipia bando ili kuweza pata huduma zao.

Huwa tunasema SIM Card bila kujua maana yake ni nini.
📡SIM ni kifupi cha Subscriber Identity Module. Ni card ambayo inatunza IMSI (International Mobile Subscriber Identity) na funguo za kumtambulisha na kumthibitisha mtumiaji katika mfumo wa mawasiliano.
📡IMSI ni namba ambayo inamtumbulisha mtumiaji yeyote wa cellular networks katika mtandao wa mawasiliano.

IMSI ni kama namba za NIDA ambazo kila mtanzania anayo yakwake. Kwenye mawasiliano kila SIM Card ina IMSI yake.
📡Sim cards zinatunza taarifa kama PIN, PUK, IMSI, taarifa za usalama na taarifa kuhusu mtandao.

Pia Sim Cards zinatunza application data ambazo zinatumika kufanya mawasiliano kati ya simu yako na server za mtandao unaotumia.
📡Hapa naongelea kitu kama SMS service number, jina la mtoaji huduma wako, namba za mtoaji huduma na vitu vingine vingi.

Sim Card yako ndicho kiunganishi kati ya simu na akaunti yako kwa mtoa huduma wako. Kiufupi ni kwamba sim card ndiyo inakuunganisha na mitandao.
📡Ninapoongelea akaunti yako kwa mtoa huduma inajumuisha kiasi gani unatumia mtandao wao, mahali ulipo, kiasi cha SMS unazotuma, muda wa maongezi na ni aina gani ya vifurushi/huduma zao unatumia.
📡Hizi ni taarifa ambazo hazipo kwenye simu yako wala Sim Card. Zinatunzwa katika database ya mtoa huduma wako kwenye server zao.
📡Kwa kumaliza niseme kwamba Sim Card ndiyo mlango wa wewe kutumia mtandao kwa namna yoyote ile. Bila Sim Card antenna za simu yako zitadaka radio waves za cellular network na hazitajua zifanye nini na mawimbi hayo.
📡Ni sawa na kuwa mtu mweusi usiyekuwa na utaifa. Utazurula sana bila kukubalika kihalali katika Nchi yoyote ya Afrika.

Unapowasha simu yako Sim card yako inaanza kutafuta mtandao wa kutumia. Hapo ndipo inachambua katika zile radio waves ni mtandao upi unatumika kwako.
📡Bila sim cards Simu yako haiwezi elewa ni radio wave ipi itumike kwako, unapokuwa na sim card sasa ndipo zile taarifa zote ndani ya sim card zinatumika.

Taarifa za jina la mtandao, SMSC na taarifa nyingine za mtoa huduma zinatumika kukuunganisha wewe na mtandao wako.
📡Nilipoongelea base station nilisema kila mtandao unabase station (mnara) yake.

Tufanye unatumia Tigo. Utakapokuwa eneo ambalo hakuna mnara wa tigo unafikisha mawimbi eneo hilo sim card yako itashindwa kutambua ijiunge na mtandao upi.
📡Hapa huwa tunasema, “Sipati mtandao, bars zipo chini kabisa.”. Ndo inakuwa kwamba Sim card imeshindwa kupata mtandao wake husika.

Kulingana na taarifa ilizotunza hakuna mtandao unaendana nazo.
📡Mnara unapopokea ombi la sim card yako kutumia mtandao wake unatumia IMSI yako kuhakikisha kama upo kwenye mnara sahihi na Sim Card yako imethibitishwa kutumia mtandao huo kwa kutumia ule ufunguo wa uthibitisho.
📡Ili kuhakikisha mawasiliano yako yanakuwa salama kuna mfumo wa usalama hapa huwa unatumika.

Mnara utakapo ikuta IMSI yako kwenye rekodi za mtandao itakuthibisha kwa kukutumia funguo. Tuite hii funguo A. Hizi funguo ni copy ya maneno flani ambayo sio rahisi kuyaelewa kibinadam.
📡Baada ya kukuthibitisha kwa funguo A, itatengenezwa funguo nyingine kwa ajili ya mnara tuite Funguo B.

Funguo B itatumwa kuja kwenye simu yako pamoja na funguo A ya uthibitisho. Simu yako itahakikisha funguo A na kutengeneza funguo nyingie C.
📡Funguo C itatumwa kurudi kwenye mtandao pamoja na ile funguo A. Mtandao utaziangalia funguo B & C, kisha kwa kutumia funguo A itahakikisha kwamba funguo B & C zinaendana.

Zikifanana hizo funguo simu yako itapata ruhusa ya kutumia mtandao ambao sim card yako iliomba kutumia.
📡Huu mfumo wa usalama ni ili kuhakikisha hakuna mtu mwingine atatumia namba yako kutumia mtandao, na hizi funguo huwa hazijirudii kwa mtu yeyote. Zikiwa tofauti utakuwa na Sim Card isiyoweza kupata mtandao.

Kwa maelekezo mepesi hivyo ndivyo Sim Card inafanya kazi.

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with HabariTech

HabariTech Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @HabariTech

15 Oct
📡A.I inajifunza kujitengeneza Yenyewe

Hofu kubwa ya watu duniani ni kuona AI ikiiteka dunia na binadamu tukawa ni watumwa wa AI.

Wenye hofu wengi ni watazamaji wa filamu kama Terminator, iRobot, Transcendence na Matrix.

#HabariTech
📡Lakini wengine ni wale wenye hofu ya kupoteza kazi zao, hasa madereva.

Hakuna wa kumlaumu mtu anayeiogopa AI kwa sababu ni kitu ambacho hata baadhi ya watu wa teknolojia wanashindwa kuelewa vizuri.
📡Miaka 2 iliyopita ungeniuliza iwapo kuna siku AI itaiteka dunia, ningejibu hiv, “Inawezekana iwapo tu tutafikia uwezo wa watu kama Tony Stark wa Iron Man.

Leo baada ya kuelewa AI kidogo nitajibu hivi, “Chochote kinawezekana na haina maana tuache kuboresha kwa sababu ya uoga.”
Read 17 tweets
12 Oct
📡Mass Surveillance Afrika na Duniani kote.

Huu ni uchunguzi ambao unajikita kufatilia umati mkubwa wa watu na mara nyingi huwa kwa kigezo cha kupunguza uharifu na kuzuia ugaidi.

Mass surveillance inasemakana kuanza miaka ya 3800 kabla ya kristo huko Babylon.

#HabariTech Image
📡Kwa vizazi vya sasa Mass Surveillance haikuonekana mpaka miaka ya mwisho ya 1940s baada ya UK na USA walikubaliana kubadilishana taarifa za intelejensia.

Baadae katika makubaliano haya ziliongezeka Canada, Australia na New Zealand na kufanya muunganiko huu kuitwa “Five Eyes”. Image
📡Muungano huu baadae mwaka 1971 ulileta kitu kilichoitwa “Global Surveillance Network” ambayo ilipewa jina la “ECHELON”.

ECHELON ni mtandao maalum wa uliofuatilia mawasiliano ya kijeshi na kidiplomati ya Soviet Union na washirika wake wa Mashariki kipindi cha Vita Baridi. Image
Read 19 tweets
11 Oct
📡Hakuna Tesla iliyotengenezwa China kuingia nchini India.

Hivi karibuni waziri wa usafiri wa barabara nchini India amesem, aliongea na Elon Musk na kumuomba kwamba Tesla kwa za india zitengenezwe nchini India.

Maalumu kabisa hakutaka Tesla za China kuwepo India.

#HabariTech
📡Akongea katika "India Today Conclave 2021", waziri huyo alisema kwamba, Gari za umeme zilizoundwa na Tata Mottors zina ubora unaokaribiana na zile za Tesla.

Hivyo Tesla za kuuzwa India inabidi zitengenezwa ndani ya India na sio China na kuuzwa kutoka India kwenda nchi jirani.
📡Sambamba na hilo alisisitiza kuwa, Tesla watapata sapoti yoyote wanayohitaji kutoka serikali ya India.

Tesla waliomba kupata punguzo la ushuru wa kuingiza gari za umeme India. Mpaka sasa hawajafikia muafaka na serikali ya India kuhusiana na maombi haya yote.
Read 5 tweets
8 Oct
📡Zima hizi settings za windows 10 haraka sana

5 Oct Microsoft waliachia windows 11, lakini hatutegemei watumiaji wake watakuwa wengi kwa sababu ya vigezo vinavyohitajika kuweza tumia Windows 11.

Kuna zaidi ya PC 1 billion zinazotumia windows 10 mpaka sasa duniani.

#HabariTech Image
📡Kati ya watumiaji hawa kuna wengi wasiofahamu baadhi ya settings ambazo zinakusanya taarufa zao, zinawafanya waone matangazo mengi au kufanya PC zao ziwe pole pole.

Ukiacha madhaifu ubora wa Win10 ukilinganisha na zile za nyuma, bado ina madhaifu mengi unakutana nayo kila siku Image
📡Kati ya hayo ni pamoja na kutokuwa na uhuru wa usiri (Privacy) wako, spidi ya OS na urahisi wa kutumia.

Leo tuchambue baadhi ya settings ambazo ni vyema ukaziweka off ili uendelee kutumia Win10 yako kwa raha.
Read 21 tweets
28 Sep
Unaijua simu isiyo na tundu la chaji wa earphone?

Ni kama uhalifu vile namna kampuni za simu zinaleta mabadiliko mapya kila kukicha.

Apple alianza kwa ondoa headphone jack kwenye iPhone 7 na matoleo yaliyofuata na baadae Samsung akafuata.

Kuna cha zaidi? Ndiyo 🧵

#HabariTech
📡Watazamaji wa Sci-Fi movies mtakuwa mmewahi kutana na zile simu ambazo ni kioo tu lakini zinafanya kila kitu.

Huenda huko ni mbali sana kufika labda 2050 huko. Twende mpaka 2030 ambapo nadhani huenda tutakuwa na simu zisizo na button yoyote, headphone jack wala tundu la chaji.
📡Unakumbuka iPhone X ilikuja na notch 2017? ikawa mwanzo wa kubadili muundo wa display za simu. Hapo tayari iPhone hazikuwa na port ya earphone

Oppo F9 ikawa simu ya kwanza kuja na teardrop screen na kumpa mtumiaji nafasi ya kutumia screen nzima.

Na sasa kuna Hole Punch.
Read 17 tweets
18 Sep
Njia rahisi kutunza UZI za twitter uweze zisoma kwa muda wako.

Twitter ni social media pendwa ambayo uhusiano wa watu unaendeshwa kwa mazungumzo ya tweets. Tweets zimekaa kwenye muundo rahisi mtu kusoma.

Bahati mbaya ni rahisi pia tweet kukupotea kama hukuitunza.

🧵#HabariTech
Ushakutana na uzi za @JemsiMunisi au @TOTTechs ?

Unakuta ni uzi flani hivi zina flow matata. Unajiuliza sasa zikipotea hizi nazipata vipi tena?

Usipate tabu tena. Leo nitakupa njia 5 ambazo zinaweza kukusaidia kutunza tweets/uzi unazokutana nazo hapa twitter.

Kana flow eeh!
1. Twitter Bookmark

Hii feature watumiaji wengi wa twitter huwa hawazingatii au hawaijui. Kwa wanaoijua ukifungua bookmark zao utakuta madini ya kutosha huko.

Kuiweka tweet kwenye Bookmark

Gusa "Share" kwenye hiyo tweet unataka save kisha chagua "Add tweet to Bookmark".
Read 11 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!

:(