My Authors
Read all threads
"Mzalendo, nani amekupa ruhusa ya kukalia majani ya jeshi?", ilikuwa ni sauti ya amri kutoka mgongoni kwangu.
Nilitazama nyuma na kukutana na kijana mrefu, maji ya kunde, mkakamavu, sura ya kazi kwelikweli.
Nikainuka, nikamtazama nisijue la kusema. FUATILIA #UZI
#DaktariMwandishi Image
Ilikuwa ndio dakika chache baada ya kuwasili Maramba JKT 838KJ, nikiwa nasubiria kukabidhi simu na ufanyiwa usajili.
Nikamsikia Afande akimuita yule aliyenisemesha, "Mbise, yatupie taulo baba."
Na huyo ndiye Afande wa kwanza kumfahamu, Afande Mbise.
Yeye ndiye aliyepewa jukumu la
kutusimamia sisi wazalendo.
Ilikuwa jioni, baada ya kukabidhiwa sehemu ya kulala na kula chakula cha usiku, Matron alitupeleka moja kwa moja hadi "uwanja wa damu", mbele alisimama yule kijana, Afande Mbise akiimbisha 'chenja'(nyimbo) mbalimbali za jeshi.
Moyoni nilikuwa na hofu
iliyochanganyika na furaha ya kwenda jeshini.
Na kwa sauti ya ukakamavu aliimba, "Lelelele amba, lelelele amba. Amba nalia, Amba lelelele amba. Amba nipo depo, amba lelelele amba."
Alikuwa na nyimbo zake alizopenda kwa mfuatano uleule.
Akimaliza "Amba", alifuata, "Aidama yoyoyoo"
Kisha "Senene senene senene, senene ni tamu kuliko nyama ukila" na kumalizia na "Sina patinaaa, ooh sina, sina patina, nalala peke yangu"
Alikuwa mkali, wengi tulimuogopa.
Wiki zilikatika, tukiwa kwenye kombania zetu, hadi siku maafande wa kombania walipobadilishwa akaletwa Dcoy
ndipo nikakutana naye kwa mara nyingine.
Alitupa kazi kweli kweli. Madoso kama kawaida.
Naikumbuka siku ile, tumekunja ngumi, pushups za uganda juu, kwa dakika nyingi na hakika nilikuwa nimefika mwisho.
Mikono ilitetemeka, jasho jembamba lilitiririka usoni na kulowesha mchanga
nikataka kuachilia, nikaisikia sauti yake, "We kamama wewe, kunja ngumi."
Nikajitahidi lakini mwili ulikuwa umeshagoma, nikajiachia kama mzigo chini.
"Unakunja ngumi au nikubadilishie zoezi", akaniuliza.
Nikafikiria naweza kukubali kubadilishiwa zoezi halafu likawa gumu zaidi.
Nikapiga moyo konde, sikuwa tayari kuendelea kupiga pushup pale mikono na miguu yote ilikuwa haina nguvu.
Kwa uoga nikasema, "nibadilishie zoezi afande."
Akauliza, "una uhakika?"
Nikasema, "ndio Afande"
Akasema, "haya nenda platuni namba 3 kaweke chenja ya morali"
Hilo likawa ndo
zoezi langu.
Nikamshukuru sana kimoyomoyo siku ile kwasababu kwakweli aliniokoa.
Siku zikayoyoma, tukamaliza kozi.
Siku ya kuondoka, nikaonana naye. Nikamkushukuru kwa miezi mitatu ya kujifunza mengi.
Sikuonana naye tena.
Tukawasiliana mara kwa mara kwenye whatsapp group, alikuwa
amehamishwa kituo.
Mambo yalikuwa yanamuendea vema, alikuwa anajiendeleza kikazi.
Ilikuwa 2016, siku kama ya leo, SABA SABA, nikapokea taarifa kutoka kwa Afande Matron mmoja ameandika, "Rest In Piece Mbise"
Nilipouliza, nikaambiwa alipata ajali.
Tulisikitika sana. Mbise hakuwa
nasi tena. Aliacha mke na watoto wadogo. Ilikuwa simanzi.
Sikuamini kwasababu nilitoka kuwasiliana naye masaa machache yaliyopita, akinieleza namna ya kujiunga jeshi na nafasi mbalimbali, wakati huo bado nina moto wa kurudi kulisaka "BakaBaka"
Hatukuwa naye tena.
Nyota imezimika.
Nikapita ukurasa wake wa Facebook, moyoni nikiimba ule wimbo wake pendwa, machozi yakinilenga, "Lelelele Amba, Lelelele Amba. Amba naliaaa, Amba lelelele Amba."
Huyu alitulea tangu tukiwa wazalendo siku ya kwanza hadi siku tumemaliza kozi.
Aliacha alama maishani mwetu hakika.
Leo, nimeketi kitandani, ni mwaka wa 4 huu bila Afande Mbise, nausikiliza wimbo wa DazNundaz, KAMANDA.
"Alazwe Pema Peponi Kamanda", mashairi haya nayaelekeza kwa Marehemu Mbise.
Aamuaye ndo Mola, hawezi kukosea.
Lala Salama.
Tutakukumbuka Daima. @KachiwilePaul
#DaktariMwandishi Image
Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh.

Keep Current with Kuduishe Kisowile

Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

Twitter may remove this content at anytime, convert it as a PDF, save and print for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video

1) Follow Thread Reader App on Twitter so you can easily mention us!

2) Go to a Twitter thread (series of Tweets by the same owner) and mention us with a keyword "unroll" @threadreaderapp unroll

You can practice here first or read more on our help page!

Follow Us on Twitter!

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3.00/month or $30.00/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!