My Authors
Read all threads
HERD IMMUNITY (KINGA JAMII/KINGA KUNDI) kutumika kupambana na COVID19 ni mjadala unoaendelea duniani, katika kipindi hiki ambacho dunia inazunguka kwenye mhimili wa janga la #COVID19, hasa katika nchi zinazoendelea ambapo "lockdown" imeonekana kushindikana. #UZI
#DaktariMwandishi
🔅Kinga jamii (Herd immunity) inatokeaje?
Asilimia kubwa ya watu katika jamii wanapokuwa na kinga dhidi ya ugonjwa fulani, wanawalinda wale wachache wasio na kinga hivyo ugonjwa unapotea.
Kwa kielelezo cha picha hapo chini, wenye mwamvuli ana kinga, asiye nao hana kinga. Hivyo
wakisimama pamoja na kuunganisha miamvuli yao, wale wasio na miamvuli hawalowi (hawapati maambukizi).

🔅Unapataje kinga jamii?
Kwa kutegemea chanjo au kinga mwili ya asili.
Magonjwa mengi yamepotea au yamekuwa adimu kwa kupitia njia hii. Lakini kwa CHANJO, sio kwa kutegemea
kinga mwili ya asili. Mpango wa taifa na kimataifa wa chanjo kwa watoto umepunguza idadi kubwa ya magonjwa kama Surua, Pepopunda n.k

🔅Unapataje kinga mwili ya asili?
Unapoumwa, mwili wako unatengeneza protini ziitwazo "antibodies" ambazo zinapigana na vimelea vya magonjwa,
protini hizi zinaulinda mwili dhidi ya maradhi.
Mwili una njia nyingi nyingine za kushambulia vimelea, na kwa pamoja zinawezesha kuushinda ugonjwa.

🔅COVID19 na HERD IMMUNITY
Wakati huu wanasayansi wanahaha kupata chanjo ya COVID19, hivyo kupata Kinga jamii kwa kutumia chanjo si
leo wala kesho.
Wanaodhani tutumia KINGA JAMII inamaanisha tutegemee KINGA MWILI YA ASILI kwa sasa.

🔅Tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa ili jamii ipate Kinga jamii kwa kupitia kinga mwili ya asili, inabidi 70-90% ya watu waugue ugonjwa huu. Kati yao 10-20% watapata madhara
makali na kuhitaji kulazwa na wengine kufariki.

🔅Je, nani anaweza kujenga kinga mwili ya asili dhidi ya COVID19?
Yeyote, lakini watu wenye kinga dhaifu wapo kwenye hatari kubwa ya kupata madhara makali ukilinganisha na wale wenye kinga ya kutosha wanapoambukizwa COVID19.
🔅TATIZO LIKO WAPI SASA? KWANINI TUSIFUATE NJIA HII?
KINGA (IMMUNITY) ya mwili inajengwa na vitu vingi na kwa muda mrefu. Daktari mmoja alisema "Kinga mwili sio nguvu za kiume kuwa utakunywa kidonge iongezeke papo hapo"
Fahamu, kwasababu hupati magonjwa mara kwa mara haimaanishi
kuwa una kinga madhubuti.

Nchi zinazoendelea zina vitu vifuatavyo ambavyo vinatishia kinga mwilini:
📌UTAPIAMLO - Hili si tatizo kwa watoto tu, hata kwa watu wazima. Kuanzia kwashakoo hadi uzito uliopitiliza, vyote vinakuweka hatarini kuwa na kinga dhaifu.
Hili ni tatizo kubwa.
📌KIFUA KIKUU - hizi nchi ndio zinaongoza kwa maambukizi ya TB ambayo hutokea kwa watu ambao wana kinga dhaifu, je watahimili COVID19?

📌UNYWAJI POMBE ULIOPITILIZA - Kiasi, aina na mlo unaoambatana na pombe vinaamua kama mwili wako utamaintain kinga au la.
📌UVUTAJI WA SIGARA, TUMBAKU NA MADAWA YA KULEVYA - Wavutaji wa sigara na tumbaku tayari wapo kwenye hatari ya kupata madhara makubwa yatokanayo na COVID19. Madawa ya kulevya hushusha kiasi cha kinga mwilini na kumweka mtu kwenye hatari ya kupata magonjwa shambulizi.
📌UKIMWI - kuna wengi wanaoishi na VVU ambao hawafahamu na hawatumii dawa, hawa wana Upungufu wa Kinga Mwilini na COVID19 ikiwapata, wataathirika.

📌SARATANI & KISUKARI- Ongezeko la magonjwa yasiyoambukizwa kwenye nchi zinazoendelea kama vile Saratani na Kisukari inashusha kinga
mwilini na kuwaweka kwenye hatari zaidi.

📌UTAMADUNI WA KUFUATILIA AFYA ZETU - Nchi zinazoendelea hazina utaamduni huu, hivyo uwezekano wa kuwa na watu wengi wenye magonjwa kama Saratani, Kisukari, UKIMWI ambayo yaanchangia kudhoofisha kinga lakini hawafahamu ni mkubwa.
📌MFUMO WA AFYA - Nchi inapoamua kuchukua njia hii, inabidi iwe na mfumo wa afya wenye uwezo wa kuhimili kuhudumia 10-20% ya wananchi wote watakaopata madhara makali ya COVID19 kwa wakati mmoja, bila kusitisha huduma nyingine za Afya.
Inajumuisha uwepo wa vyumba vya wagonjwa
mahututi, mashine za upumuaji, oksijeni, wafanyakazi wa kutosha, vifaa vya kujilinda na vingine vingi.
Na hivi vyote visicompromise huduma nyingine za afya kwa wagonjwa wa magonjwa mengine.

Wengi wanasema "Mbona Sweden wameweza?"
Hali ya COVID19 Sweden siku chache zilizopita:
Hiyo ni kwa nchi ambayo ina kati ya mifumo mizuri zaidi ya afya duniani. Sijui kwa nchi inayoendelea.

🔅Watafiti wamejaribu kufuatilia uwezekano wa kutoa vyeti vya kinga dhidi ya COVID19 lakini kutokana na tafiti zilizofanyika hadi sasa kupitia kupima kiasi cha antibodies baada
ya maambukizi, wameona kuwa:
📌Watu tofauti wanatengeneza kiasi tofauti cha antibodies
📌Haijulikani kiasi gani cha antibodies kinahitajika kujenga kinga mwili imara kiasi cha kutokupata maambukizi ya COVID19 tena.
📌Vipimo vya antibodies vinavyotumika ni tofauti
🔅Lakini zaidi, Korea Kusini imepata watu ambao walionekana kupona kabisa wakapata maambukizi tena. Wiki chache zilizopita, ilikuwa 2% ya waliopona walipata maambukizi tena.
Hivyo, inaibua maswali kwamba je, KINGA JAMII inaweza kupatikana?

🔅Virusi vinabadilika (MUTATION)
ili kuendana na mazingira, hili nalo linaleta ukakasi kuwa, je, virusi hivi vinbadilika haraka kiasi gani na je, mtu anapotengeneza kinga dhidi yake, kikibadilika uwezo wa kupata maambukizi tena upoje?

📌USUGU WA VIMELEA (ANTIMICROBIAL RESISTANCE)- Tatizo kubwa duniani ambalo
nalo linaongeza hatari zaidi ya maambukizi na kuleta chalenge kwenye matibabu.

🔅Ni kweli, tunaweza kupata kinga jamii lakini kwa bei gani?
Wakati Uingereza wameanza na njia hii, kiongozi wao mmoja alisema, "Baadhi ya wapendwa wenu watafariki"
Je, upo tayari kuwa kati yao?
Uingereza kwa sasa wamebadili njia baada ya mlipuko kuongezeka kwa kasi na hata Waziri Mkuu na Mtoto wa Malkia kupatwa na ugonjwa huu.
Infikirisha.

Unapoamua kutumia kinga jamii kwa kutegemea kinga mwili ya asili, inamaanisha wapo watakaofariki, wanaweza kuwa wengi, sana.
Ni kama mchezo wa kamari. Lakini uwezekano wa kuliwa ni mkubwa zaidi.

🔅Hatari nyingine ya njia hii ni hospitali kufurika na kuelekeza nguvu kwenye COVID19 hivyo kusababisha vifo vya waathirika wa magonjwa mengine ambavyo vingezuilika. Kuchukua njia hii, Jipange Sawasawa.
🔅Inawezekana ikafanya kazi, hakuna anayejua.
Ni mchezo wa pata potea.
Mchezo hatari.
Mara nyingi wanaosema tuitumie hii, hawadhani kama watakuwa kati ya watakaopata madhara makali au watakaofariki.
Boris baada ya kulazwa ICU, mawazo yalibadilika.
🔅Iwapo ikafanya kazi bila madhara yote haya, kuna uwezekano wa hali kurudi kawaida mapema.
🔅Iwapo haitofanya kazi, uchumi utadorora zaidi, kwani nguvukazi itapotea, hospitali zitazidiwa na fedha nyingi zitaelekea huko.
Hiyo ndio hofu kubwa, mochwari zisipotosha, itatisha.
🔅Kukabiliana na COVID19:
📌VIFAA VYA KUJILINDA KWA WAFANYAKAZI WA AFYA
📌Nawa mikono
📌Epuka mikusanyiko
📌Vaa barakoa
📌Safisha nyuso (surfaces) za vitu
📌Elimu kwa jamii
📌Uonapo dalili, toa taarifa mamlaka husika
📌Usisambaze taarifa POTOFU
NAWASILISHA!
#DaktariMwandishi 👣
@threadreaderapp unroll please
Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh.

Enjoying this thread?

Keep Current with Kuduishe Kisowile

Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

Twitter may remove this content at anytime, convert it as a PDF, save and print for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video

1) Follow Thread Reader App on Twitter so you can easily mention us!

2) Go to a Twitter thread (series of Tweets by the same owner) and mention us with a keyword "unroll" @threadreaderapp unroll

You can practice here first or read more on our help page!

Follow Us on Twitter!

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3.00/month or $30.00/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!