FAHAMU MVUMBUZI WA TELEVISION (📺)

#Yes_____&&
#Thread|story🕐
Any sufficiently Advanced Technology is indistinguishable from MAGIC!! Binafsi huwa nasema Technology Is the Great ant💉dote to the Poison of Enthusiasm and Superstition💣
📋Asili ya TV
📋Historia yake
📋Uvumbuzi n.k
Televisheni (TV) au Runinga ni kifaa chenye kioo ambacho kinapokea mawasiliano kutoka kituo cha televisheni na kuyabadilisha kuwa picha na sauti.

Neno "Televisheni" linatokana na maneno mawili:
(i)Tele (Kigiriki)-kwa mbali sana na
(ii)Visio (Kilatini)-mwono.

RT @omari_manyama
kwa pamoja yanaunda neno la Kiingereza #Television limetoholewa kwa lugha ya Kiswahili "Televisheni".

Ugunduzi wa TV📺 ni kazi iliyofanywa na watu wengi mwishoni mwa karne ya 19.Karne ya 20 Watu mmoja-mmoja na makampuni yalishindana kuunda chombo kilichopiku teknolojia ya awali.
Wengi walisukumwa kuwekeza mitaji ktk ugunduzi huo na kupata faida huku wengine wakitaka kuubadili ulimwengu kwa njia ya teknolojia ya mawasiliano ya kuona na kusikia kwa wkt mmoja. Hayupo mtu mmoja wa kupewa sifa pekeake kwa uvumbuzi wa 📺, kila mmoja alifanya kwa uwezo wake.!!
Wazo hilo lilikuwa likizunguka muda mrefu kabla teknolojia haijawahi kutokea, na wanasayansi na wahandisi wengi walitoa michango yao ambayo ilijengwa kwa kila mmoja hatimaye kutoa kile tunachojua kama Runinga ya leo.
Asili ya TV inaweza kufuatiwa hadi miaka ya 1830's na 1840's, wakati SAMUEL F.B. MORSE alipotengeneza mfumo wa kutuma ujumbe uliotafsiriwa kwa sauti (Telegraph) ktk uzi au waya. ALEXANDER BAIN ndiye aliyeanzisha mtambo wa kutengeneza kivuli cha picha baina ya mwaka 1843/46.
Mfumo wa kwanza wa kivuli cha picha kufanyiwa kazi kwa mistari ya telegrafu uliendelezwa na kuingizwa kazini na Giovanni Caselli kuanzia mwaka 1856 na kuendelea. Willoughby Smith akatengeneza mkondo wa picha wa kifaa cha selenium mwaka 1873.
Hatua nyingine muhimu mbele ilikuja mnamo 1876 ambapo Alexander Graham Bell alitengeneza mtambo wenye kama mfumo wa simu ambayo iliruhusu sauti ya mwanadamu kusafiri kupitia waya kwa umbali mrefu zaidi
Alexander Bell na Thomas Edisons waliamua juu ya uwezekano wa kutengeneza kifaa kama simu ambacho kinaweza kusambaza picha na sauti. Baadae mtafiti mmoja wa Ujerumani ndiye aliyechukua hatua iliyofuata kuelekea kukuza teknolojia iliyowezesha runinga.
Rt @balozi_twita @Kiganyi_
Mnamo 1884, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ujerumani, Paul Julius Gottlieb Nipkow akiwa na umri wa miaka 23, alibuni na kutengeneza kitu km sahani iliyoitwa "Nipkow disk" iliyokuwa na mfumo wa kutuma picha kupitia diski inayozunguka ktk waya, akaiita "Electronic telescope"
Hii ilikuwa ni santuri ya kuzunguuka ikiwa na matundu ya duara ndani yake, kila tundu likifanya mstari wa picha. Japo yeye hakujenga modeli ya utendajikazi ya mfumo huo lakini aina mbalimbali za santuri ya Nipkow zikawa mashuhuri mno.
Constatin Perskyi ndiye aliyebuni neno #Television katika andiko lililowasilishwa ktk Mkutano wa Umeme wa Kimataifa kwenye maonesho ya kimataifa mjini Paris, Agosti 25, 1900. Andiko la Perskyi lilipitia upya teknolojia zilizokuwepo za nguvu ya umeme wa mitambo.
RT @Vet_doctor87
Mwanzoni mwa 1900, mwanafizikia wa Kirusi Boris Rosing na mhandisi wa Uskoti Alan Archibald Campbell-Swinton walifanya kazi kwa kujitegemea kuboresha mfumo wa Nipkow kwa kubadilisha diski zinazozunguka na kuwekwa ktk kiwambo cha Cathode tube.
Teknolojia hiyo iliboreshwa zaidi na mwanafizikia wa Ujerumani #Karl_Braun.

Mfumo huo wa Swinton, ndio ambao uliweka mirija ya cathode ndani ya kamera iliyotuma picha iliyokuwa inafanana na ile inayotolewa na mpokeaji, na kimsingi huu ndio ulikuwa mfumo wa kwanza wa televisheni
Hata hivyo, waliendelea kupambana ili kitu cha maana zaidi ktk mawasiliano na mnamo mwaka 1907, maendeleo ya teknolojia ya mtambo wa kukuza sauti yalipofikiwa na Lee de Forest ambapo Arthur Korn pamoja na wengine walifanya muundo huo kuanza kazi
Kuonekana kwa mawasiliano rasmi ya picha kulifanywa kwa mara ya kwanza na Rignoux na A. Fournier mnamo mwaka 1909. Mpangilio (matrix) wa vibetri vidogo vidogo vipatavyo 64, kila kimoja kikiwa kimeunganishwa waya katika mtambo endeshi ndivyo vilivyofanya kazi kama retina ya jicho.
Katika kipokezi, aina ya kibetri cha Kerr cell ndicho kiliratibu mwanga na milolongo ya vioo mbalimbali vya pembeni vilivyoambatanishwa na ukingo wa sahani inayozunguka (santuri) ikigagamiza mwangaza hadi ndani ya kioo cha luninga.
Mfumo maalum wa umeme ndio ulioratibu utendajikazi wa pamoja wa chombo hicho. Kioo cha ukubwa wa nane kwa nane katika mtambo huo wa runinga kilitosha kuwasilisha herufi za maneno pamoja picha ilionekana mara kadhaa kwa kila sekunde.
Mnamo mwaka 1911, Boris Rosing na mwanafunzi wake Vladmir Zworykin walibuni mfumo ambao ulitumia kigagamizi cha ngoma ya kioo ambacho, kwa maneno ya Zworykin, kilileta picha chafu sana kwa waya uliounganishwa na muanzi wa mwangaza ndani ya kipokezi.
Huyu Vladimir Zworykin alizaliwa Urusi na alikuwa akifanya kazi kama msaidizi ktk kampuni ya Boss wake Boris Rosing kabla ya wote kuhama kufuatia Mapinduzi ya Urusi.
Baadae Zworykin aliajiriwa katika kampuni ya utengenezaji vifaa vya kielektroniki na umeme huko Pittsburgh Westinghouse, miaka ya 1923 ambapo aliomba hati miliki ya kwanza ya runinga, kwa "Iconoscope," ambayo ilitumia mirija ya cathode ray kusambaza picha.
Kufikia 1920's, TV ilianza kufanya kazi, mgunduzi wa nchini Scotchland Bw. John Logie Baird alitumia santuri ya Nipkow ktk mifumo yake ya video.
Alitengeneza aina yake ya santuri huko Santa Cruz (Trinidad Islands). Pia aliyeanza utundu wa kubuni televisheni ya kwanza ya rangi.
Mnamo Machi 25, 1925, Baird alitoa onesho la kwanza la picha za kutembea za televisheni Jijini London. Kwa kuwa nyuso za wanadamu zilikuwa zinaoneka vizuri ktk mfumo huo duni alitengeneza sisira la kuzunguka ambalo lilitengeneza muonekano au sura yake ya mtu.
Mnamo 1929, Zworykin alionyesha mfumo wake wa elektroniki kwenye maonyesho ya wahandisi wa redio. Mojawapo waliohudhuria ktk maonyesho hayo ni David Sarnoff, Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Redio la Amerika (RCA), kampuni kubwa ya mawasiliano ya taifa wakati huo.
Mnamo Januari 26, 1926, alionesha picha ya uso. Hii ndiyo inayohesabiwa kama Televisheni ya kwanza ya kuonesha picha nzuri katika historia. Na mwaka 1929, Zworykin alionyesha mfumo wake wa elektroniki kwenye maonyesho ya wahandisi wa redio.
Mojawapo waliohudhuria ktk maonyesho hayo ni David Sarnoff, Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Redio la Amerika (RCA), kampuni kubwa ya mawasiliano ya taifa wakati huo.
Sarnoff alizaliwa ktk familia masikini ya Kiyahudi huko Minsk, Urusi, baadae akaenda New York akiwa mdogo na akaanza kazi za telegraph.
Ktk usiku wa janga meli ya #Titanic alikuwa kazini, lkn alishindwa kuratibu ujumbe wa sauti uliotumwa na meli za karibu kuomba msaada wa uokoaji
Sarnoff alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kufanikisha maendeleo ya Televisheni ya sasa ambapo baadae alimwajiri Zworykin ktk kampuni yake kukuza na kuboresha teknolojia ya runinga kwa kampuni hiyo.
Zworykin alikutana na Philo Farnsworth kijana mmoja mporipori aliyekuwa akifanya kazi RCA (kampuni ya Sarnoff) kitengo cha Television, akampa wazo la kuweka bomba la utupu ambalo litagawanya picha kuwa mistari, kisha kusambaza mistari hiyo na kuigeuza kuwa picha.
Wamarekani huamini Farnsworth ndiye mtu wa kwanza kuvumbua TV kwasababu mnamo 1927, akiwa na miaka 21, alitengeneza kitu chenye mfano wa mfumo wa kwanza wa runinga wa elektroniki unaofanya kazi kabisa. Lakini ukweli ni kuwa sio yeye maana hata ujuzi aliotumia ni wa Paul Nipkow.
Kutokana na wazo lake lile inaaminika miaka ya karibuni alijikuta akiingia kwenye mgogoro wa kisheria kwa muda mrefu na kampuni ya RCA, ambayo ilidai uvumbuzi wa Aawali wa Zworykin wa mwaka 1923 ndio ulichukuliwa kipaumbele kuliko uvumbuzi wa Farnsworth.
Rt @chapo255 @funjojr
Serikali ya Marekani iliamua mgogoro huu kwa kumpendelea Farnsworth (Mmarekani) na kipaumbele kwamba mnamo 1934 alisaidia kuwa sehemu muhimu na mvumbuzi wa television tena akiwa mdogo hivyo Sarnoff mwishowe alilazimishwa kumlipa Farnsworth US$ 1M km ada ya leseni.
Ingawa alitazamwa na wanahistoria wengi kama mwanzilishi wa runinga, lkn Farnsworth hakupata faidi zaidi kutokana na uvumbuzi wake, na alikuja kushtakiwa baada RCA kukata rufaa. Baadaye aliendelea na taaluma za utengenezaji wa silaha za nyuklia na alifariki dunia 1971 akiwa deni.
Sarnoff na kampuni yake mauzo, alitambulisha TV yenye muundo mpya na kubwa kuliko zote ktk maonyesho ya ulimwengu huko New York City mnamo 1939. Chini ya mwavuli wa RCA, kampuni ya utangazaji ya kitaifa (NBC). Alifanya ufunguzi, kisha na Rais Franklin D. Roosevelt alihutubia.
Baada ya hapo kumekuwepo na miundo mbalimbali ya TV na imekuwa ikibadilika siku hadi siku, muongo baada ya muongo mmoja, teknolojia ya Runinga imeendelea kwa kasi. Muonekano mzuri wa rangi ilivumbuliwa ktk miaka ya 1960, ikifuatiwa na cable miaka ya 1970's na VCRs miaka ya 1980's
Maendeleo zaidi ya Televisheni yenye picha angavu zaidi kwa mfumo wa High definition (HDTV) ilikuja mwishoni mwa miaka ya 90. Ktk karne ya 21, watazamaji wana uwezekano wa kutazama vipindi kwenye simu za rununu (smartphones), kompyuta ndogo km vile unavyoona ktk 📺 ya kawaida.
Leo hii kuna Televisheni za kisasa ambazo ni kubwa sana na zenye picha angavu sana.

#The End_______&&

If u Read this #Uzi kindly
JUST RETWEET and FOLLOW ME
kwa Ajili ya Kupata #Nyuzi bin #Nyuzi Everyday..!!

Thanks 🙏🙏

• • •

Missing some Tweet in this thread? You can try to force a refresh
 

Keep Current with JAPHET MATARRA

JAPHET MATARRA Profile picture

Stay in touch and get notified when new unrolls are available from this author!

Read all threads

This Thread may be Removed Anytime!

PDF

Twitter may remove this content at anytime! Save it as PDF for later use!

Try unrolling a thread yourself!

how to unroll video
  1. Follow @ThreadReaderApp to mention us!

  2. From a Twitter thread mention us with a keyword "unroll"
@threadreaderapp unroll

Practice here first or read more on our help page!

More from @Eng_Matarra

13 Jun
"YOU ARE UNDER ARREST"

#Uzi

📌Je, wajua Leo ilikuwa siku ambayo sheria inayomlinda mhumiwa [Miranda rights/Warnings] anapokamatwa na vyombo ulinzi ilipitishwa huko marekani?

💨YES it's Miranda Vs Arizona case

📌 Historia yake

📌 Chanzo chake

📌Maamuzi ya kihistoria.

👇👇 ImageImage
Mnamo Juni 13, 1966 Mahakama Kuu ya Juu (Supreme Court) nchini Marekani ilitoa uamuzi wa kihistoria juu ya taratib za uendeshaji kesi za jinai mahakamani.Uamuzi huo ulitokana na kesi ya Miranda Vs Arizona kwamba watuhumiwa wa kesi wanazo haki zao kabla ya kuhojiwa wawapo kizuizin Image
Nadhani ulishawahi kusikia maneno haya

1. Una haki ya kukaa kimya.

2. Chochote unachosema kinaweza, na kitatumika, kama ushahidi mahakamani.

3. Una haki ya kuwa na wakili.

4. Ikiwa hauwezi kumudu gharama za wakili mahakama, itamteua mmoja kusimamia kesi zako

Tuendelee 👇 Image
Read 35 tweets
8 Sep 20
FAHAMU KUHUSU JAPHET KIRILO

#Uzi

✴️Mtanzania wa Kwanza kuachia Ubunge kisa mashamba ya kahawa 1990's

✴️Akiwa 31yrs alikwenda mpk UN kutetea wakulima
✴️Huyu ndiye alisomesha Wameru wengi akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Gen. SARAKIKYA pamoja na Babaake @CarolNdosi👇
Kwanz kabisa ktk HISTORIA ya Ukombozi wa Tanganyika kutoka kwa Mkoloni Haiwezi KUMTENGA Kirilo Japhet

Tukiwa tunaendelea hapo juu Pichani ni Japhet Kirilo (kulia), akizungumza na mmoja wa viongozi wa serikali ya kikoloni Ralph Bunche..

Tuendeleeee👇👇
Katika historia kuna matukio mbalimbali yaliyofanyika kwenye taifa hili. Leo tumwangalie Kirilo Japhet ambaye alitoka katika Mkoa wa Meru (Arusha ya sasa). Historia tunayoandika hapa leo ni kutokana na andiko la kitafiti la Dk. Simeon Mesaki wa Chuo Kikuu cha Dodoma.
Read 30 tweets
6 Sep 20
FAHAMU MAANA NA ASILI YA MAJINA YA MAJIMBO YA MAREKANI

#Uzi mfupi.

Marekani ilipata uhuru wake mwaka 1776 na kuwa Jamhuri rasmi mwaka 1789, ina jumla ya majimbo 50 na jimbo la mwisho kujiunga kwenye muungano wa Marekani ni jimbo la Hawaii.
Hawaii iliingizwa kwenye shirikisho rasmi mwaka 1960 baada ya marekebisho ya 15 ya katiba ya nchi hiyo (15th ammendment) na ni zao la sheria mpya iliyoitwa Hawaii Adimision Act, yaliyofanyika mwaka 1959, ili kuingiza jimbo la Hawaii katika shilikisho la muungano wa Marekani.⠀
Hawaii ndio jimbo la mwisho kujiunga na Marekani, na kukamilisha jumla ya majimbo 50 yanayounda Taifa la Marekani/United States of America (USA), ndio maana kwenye Bendera ya Marekani uwakilishwa na nyota 50 kuashiria jumla ya nchi (majimbo) 50 yanayounda umoja wa taifa hilo.
Read 29 tweets
21 Aug 20
VISA VYA MADINI YA TANZANITE

#Thread

✴️Manuel De' Souza Fundi Cherehani na mgunduzi halisi ila hakupewa heshima,

✴️Mzee Ngoma atangazwa mgunduzi ilihali sio

Twende chap...

💨Asili ya Tanzanite
💨Historia yake
💨Visa ktk ugunduzi wake
💨Thamani yake
💨Sababu ya kuitwa hivyo👇
Kila mwaka July 07 huwa ni siku maalum na ukumbusho muhimu sana, na huwa ninafanya sherehe ya Birthday kwa ajili ya Mimi na Baba yangu (sisi wawili tulizaliwa siku hii), Lakini pia siku hii ndio madini ya Tanzanite yaligunduliwa.

Mwaka huu pia nilifanya..

Turudi ktk uzi👇
Tunapozungumzia juu ya vito vya thamani, basi fikra zetu kwa mbali hutupeleka ktk vito vya asili na bila shaka huwezi kukosa kuwazia madini ya Almasi, Emerald, Rubi na Lulu ila kama hufahamu Tanzanite ni moja ya madini ya asili na ghali sana na yenye historia tamu sana.

Twende👇
Read 58 tweets
12 Aug 20
MY LIFE

✴️TRUE STORY

#Thread...!!!👇

Leo nimeamka kukiwa na Baridi sana hapa Jijini Arusha nikakumbuka mbali (nikiwa Hamburg Ujerumani) nikawaza kushare nanyi historia ya maisha yangu itakuwa ktk sehemu Tatu
1. Sehemu I (kuzaliwa)
2. Sehemu II (Masomo)
3. Sehemu III (Maisha) Image
#SEHEMU I

Naitwa Japhet Matarra, nimezaliwa July 07, 1991 kijijini kwetu Machochwe Wilayani Serengeti.

Katika familia yetu mimi ni mtoto wa Tatu kati ya watoto 17 na FIRST BORN kwa Mama Yangu. Nilianza S/Msingi  mwaka 1998 hapo kijijini kwetu na kuhitimu Drs la VII mwaka 2005. Image
Baada ya hapo nilijiunga na masomo  ya sekondari mwaka 2006 ambapo nilichaguliwa kwenda shule ya kata (Machochwe sec) kama ilivyo kawaida vijijini na kayumba schools zetu na kuhitimu O-level mwaka 2009.

Hapa ndipo maisha yangu yalichange nitaelezea mbele ktk sehemu ya III Image
Read 163 tweets

Did Thread Reader help you today?

Support us! We are indie developers!


This site is made by just two indie developers on a laptop doing marketing, support and development! Read more about the story.

Become a Premium Member ($3/month or $30/year) and get exclusive features!

Become Premium

Too expensive? Make a small donation by buying us coffee ($5) or help with server cost ($10)

Donate via Paypal Become our Patreon

Thank you for your support!

Follow Us on Twitter!

:(